Skip to main content

DALILI ZA HATARI KWA MAMA MJAMZITO

Ujauzito huja na tabia nyingi ambazo baadhi huwa za kawaida huku baadhi zikiwa siyo za kawaida.

Ni muhimu sana kwa mama mjamzito kuzungumza na daktari mara kwa mara ili kuondoa sintofahamu hizi ambazo siyo nzuri kwa afya.




Tumekuletea dalili za hatari wakati wa ujauzito ambazo ni lazima zishughulikiwe haraka ili kuzuia madhara makubwa yanayoweza kutokea kwa mama na mtoto.

1. Damu kwenye via vya uzazi
Katika mazingira ya kawaida, damu huwa haipaswi kutoka wakati wote wa ujauzito.

Katika mazingira fulani, siku ya 10-14 baada ya kutungwa kwa ujauzito mwanamke anaweza kutokwa na damu kidogo ambayo humaanisha kuwa kijusi kinajishikiza kwenye mji wa uzazi ili kianze kulelewa.

Kutokwa na damu kwenye via vya uzazi muda wowote mwingine siyo ishara nzuri hivyo inapawa kuchukuliwa kama jambo la dharura.

Baadhi ya sababu zinazoweza kufanya damu itoke ni uwepo wa maambukizi makubwa, tishio la kuharibika kwa ujauzito, kuwa na ujauzito unaolelewa nje ya mji wa uzazi au uwepo wa changamoto zozote kwenye kondo la uzazi.

2. Kifafa na degedege
Shinikizo la juu la damu wakati wa ujauzito ambalo huambatana na uwepo wa protini kwenye mkojo husababisha kifafa cha ujauzito.

Hali hii ya kifafa na degedege huwa ni hatari kwa afya ya mama na mtoto.

Inaweza kusababisha kifo cha mama au mtoto, kuharibika kwa ujauzito, kujifungua kabla ya wakati, kuathiri mfumo wa fahamu, kuharibu viungo vya mwili, upofu pamoja na kujifungua watoto wenye tatizo la degedege.

3. Kichwa na macho
Maumivu makali ya kichwa na kupungua uwezo wa macho kwenye kuona ni dalili za kifafa cha ujauzito.

Ni muhimu sana kwa mwanamke mjamzito kufika hospitalini haraka.

Dalili hizi mara nyingi huonekana kuanzia wiki ya 20 ya ujauzito na kuendelea.

4. Mtoto kuacha kucheza
Baadhi ya watoto huanza kucheza kuanzia wiki ya 13-16 tangu mwanamke aone hedhi yake ya mwisho.

Kwa wanawake wenye ujauzito wa kwanza wanaweza kuchelewa hadi wiki ya 18-20 ndipo wahisi miondoko ya mtoto.

Kwa kuwa kila mwanamke hupata ujauzito kwa namna yake, wastani wa muda wa kawaida wa kuanza kucheza kwa mtoto huwa ni kuanzia wiki ya 13-25.

Kama mtoto alikuwa kazoea kucheza kisha akaacha ghalfa, unapaswa kuwa na wasiwasi maana hii siyo ishara nzuri.

Fika hospitalini kwa uchunguzi ili kufahamu kama tukio hili lina maana nzuri au mbaya.

5. Maumivu makali tumboni
Maumivu makali ya tumbo hasa yale yanayotokea kwenye sehemu ya chini ya tumbo huwa siyo mazuri.

Maumivu haya yanaweza kuambatana na hali ya kukaza kwa misuli ya tumbo.

Yanaweza kuwa na maana kuwa mwanamke anataka kupatwa na uchungu wa mapema kabla ya muda halisi.

Ni muhimu kufika hospitalini kwa uchunguzi na matibabu.

6. Kupasuka kwa chupa
Mtoto huhifadhiwa kwenye nyumba ya uzazi ambayo kwa lugha rahisi inayofahamika zaidi huitwa chupa ya uzazi.

Chupa hii haipaswi kupasuka muda wowote ule kabla ya uchungu wa kuzaa.

Wastani wa asilimia 3-10 ya wanawake wote wanaojifungua.

Kupasuka kwa chupa ya uzazi kabla ya siku sahihi ya uchungu husababisha maambukizi kwa mama na mtoto, kunyofoka kwa kondo la uzazi pamoja na changamoto kwenye kitovu.

Ni muhimu kufika hospitalini ili tiba sahihi iweze kutolewa.

Inaweza kuhusisha matumizi ya dawa, sindano au kuzalishwa haraka ikiwa ujauzito utakuwa umefikia kwenye hatua ambayo mtoto akitolewa ataweza kuishi.

7. Homa kali
Kupanda kwa joto hadi 100.4°F (38°C) siyo jambo zuri kutokea wakati wa ujauzito.

Homa hii inaweza kuwa hatari zaidi kama itaambatana na kiungulia, kuhara, maumivu makali ya tumbo na mgongo, kupungua kwa mkojo pamoja na kutokwa na uchafu ukeni wenye rangi na hatufu kali.

Inaweza kuwa ishara ya uwepo wa maambukizi makali kwenye sehemu mbalimbali za mwili hasa zile zinazohusisha figo, mji wa uzazi au mapafu.

8. Maumivu ya kifua
Katika mazingira ya kawaida, maumivu ya kifua wakati wa ujauzito huwa hayana maana mbaya.

Husababishwa na kiungulia, au mgandamizo mkubwa unaofanywa na mtoto kwenye kusukuma viungo vya mwili kuelekea nafasi ya wazi ya kifua.

Hali inaweza isiwe ya kawaida kama maumivu haya ya kufua yataambatana na changamoto za kupumua pamoja na kuongezeka kwa mapigo ya moyo.

Uchunguzi wa haraka unahitajika.

9. Uvimbe
Kuvimba kwa mwili wakati wa ujauzito (Edema) ni jambo linalotokea kwa wanawake wengi. Uvimbe huu mara nyingi hutokea kwenye mikono, miguu, uso na maungio ya mifupa.

Hata hivyo, katika nyakati chache, kuvimba kwa mwili kunaweza kuwa dalili mbaya ya uwepo wa changamoto kubwa za kiafya hasa shinikizo kubwa la damu linaloweza kuleta kifafa cha mimba pamoja na kuganda kwa damu kwenye mishipa ya damu maarufu zaidi kama deep vein thrombosis (DVT) ambayo ni chanzo cha kiharusi.

Ni muhimu kufika hospitalini haraka kwa ajili ya uchunguzi na matibabu.

Ikiwa ujauzito hauna tishio lolote la kuharibika, njia nzuri na rahisi ya kuzuia tatizo la kuvimba kwa mwili ni kushiriki mazoezi mepesi hasa yale ya kutembea, kufanya kazi ndogondogo za nyumbani pamoja na kuacha tabia ya kukaa (kupumzika) muda mrefu pasipo kujishughulisha na jambo lolote.


Naomba niishie hapa. Nikaribishe Maswali, Karibuni Sana..



Je, Unahitaji Kupata Huduma Kutoka Liwaya Herbal Clinic ? Basi wasiliana nasi Kwa namba hizi: 0755162724



Pia Unaweza kutembelea tovuti yetu: www.liwayaherbalclinic.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

DAWA YA KUTIBU JINO UKIWA NYUMBANI

DAWA YA KUTIBU MENO KWA HARAKA NA UHAKIKA Dawa hii imeniponesha mm mwenyewe nilikuwa nasumbuliwa na jino la juu na ndipo nilipoamua kuandaa dawa hii na imenitibu kwa HARAKA na ufanisi wa Hall ya juu sana na bado sijapatapo kuona dawa nzuri kama hii,huna haja ya kung'oa meno yako baada ya kuifahamu dawa hii eti kwasababu yanauma Mahitaji 1.✍ Mafuta ya karafuu/clove oil. 2.✍ mafuta ya Nazi/coconut oil. 3.✍ Kitunguu maji. 4.✍ Kitunguu swaum. 5.✍ Pilipili manga. 6.Chumvi ya mawe/unga wake MAANDALIZI Ponda ponda Kitunguu maji,Kitunguu swaumu,chumvi ya mawe na pilipili manga kisha changanya na mafuta na Nazi na mafuta ya karafuu kwa kiasi kidogo (robo kijiko kidogo cha chai) kisha chukua mchanganyiko huu kisha uweke juani kwa muda wa dakika 15 kisha toa juani MATUMIZI 1.ikiwa jino lina tundu chukua uji uji wa mchanganyiko huu kisha weka katika tundu na mafuta yake yapakaae pembezoni mwa jino linalouma. 2.ikiwa jina halina tundu pakaa mafuta ya mchanganyiko huu pembezoni kulizunguka jino...

TATIZO LA KUFUNGA CHOO NA KUPATA CHOO KIGUMU

Tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu ni jambo tunalolikwepa kwenye mazungumzo yetu ya kila siku. Hata hivyo ni tatizo kubwa katika jamii na mbaya zaidi wengi hawajuwi madhara yake ni nini ya kuendelea kulivumilia tatizo hili. Kupata choo kigumu au kufunga choo ni ishara ya tatizo lingine baya zaidi mwilini. Kama kuna jambo unapaswa uliepuke kwa nguvu zote basi ni hili. Kwa afya bora kabisa hakikisha unapata choo kila siku mara 2 hata mara 3. Choo kilaini siyo kigumu na chenye maumivu. Wakati mwingine utakapopata tatizo hili naomba usiwe na aibu kulisema wazi hata kwa boss wako ili upate matibabu kwa haraka. Kufunga choo au kupata choo kigumu ndiyo CHANZO KIKUU CHA UGONJWA WA BAWASIRI kwa waTanzania wengi na hii inachangiwa kwa sehemu kubwa kwa kula ugali wa sembe na kutokunywa maji mengi kila siku. Pamoja na hayo, hakuna ugonjwa rahisi kutibika kama huu ikiwa utaamua kushughulisha kichwa chako kidogo hasa kwa kuangalia unakula na kunywa nini kila siku. Inatakiwa ifahamike kuwa ...

NI KWA NAMNA GANI BACTERIA (H.pyori) Husababisha vidonda vya TUMBO

-Bacteria, Helicobacter pylori/Campilobacter pylori_* anaweza kusafiri kutoka kwa mtu Mmoja kwenda kwa mwingine kupitia njia zifuatazo: ⤵⤵⤵ (a).📎Kupitia mate (kunyonyana midomo) (b).📎Kupitia matapishi. (c).📎 Kupitia kinyesi (d).📎Kupitia chakula ama maji yaliyokuwa na bacteria hawa. SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA MTU KUAMBUKIZWA BACTERIA HAWA_ (H.pylori) ⚫ Kuishi mazingira yenye mikusanyiko mkubwa wa watu bila kuchukua tahadhar. ⚫ Kunywa maji yasiyokuwa safi. ⚫ Kula vyakula visivyooshwa mfano matunda na Mboga za majani. ⚫ Kuishi karibu na mtu mwenye vidonda vya tumbo bila kuchukua tahadhar. H.pylori anapoingia katika mwili wa binadamu huathiri uzio mwenye kulinda ukuta wa tumbo na utumbo mdogo (protective mucous) hali hii hupelekea kudhoofika kwa kuta katika tumbo na utumbo mdogo. Ukuta huu unapodhoofika husababisha Tindikali (Asidi) inayozalishwa tumbo kuunguza na kuuchimba ukuta wa tumbo pia Bacteria hawa huchimba ukuta wa tumbo na KUSABABISHA kutokea vidonda katika ukuta wa tumbo...