Skip to main content

PID,SABABU ZAKE,DALILI ZAKE,KUJIKINGA KWAKE NA MATIBABU YAKE KWA DAWA ASILI

 PID SABABU ZAKE DALILI ZAKE KUJIKINGA KWAKE NA MATIBABU YAKE KWA DAWA ASILIA


    DAWA YA PID


Pelvic Infalammatory Disease (PID) ni maambukizi kwenye viungo vya uzazi vya mwanamke. PID hutokea pale bakteria waenezwao kwa ngono wanaposambaa kutoka kwenye uke (vagina) hadi kwenye nyumba ya uzazi (uterus), mirija ya uzazi (fallopian tubes) na ovari.


Dalili za PID huweza kuwa ni ngumu kueleweka. Baadhi ya wanawake hawaoni dalili zo zote. Kwa maana hiyo, unaweza usihisi cho chote hadi pale utakaposhindwa kupata ujauzito au hadi utakapoanza kupata maumivu ya kiuno.


 



PID MAENEO YA pid


Dalili Za PID

PID inaweza isilete dalili zo zote mbaya na ndogo zikitokea zinaweza kuwa ngumu kuzigundua. Baadhi ya wanawake hawapati dalili zo zote. Pale zinapojitokeza, zinaweza kuwa:


. Maumivu – yanayoweza kuwa madogo au makali – maeneo ya chini ya tumbo au nyonga

. Uchafu usio wa kawaida au mzito ambao unaweza kuwa na harufu mbaya

. Kutokwa damu kusiko kwa kawaida, hasa wakati wa tendo la ndoa, au katikati ya siku za hedhi

. Maumivu wakati wa kujamiiana

. Homa, wakati mwingine kusikia baridi

. Maumivu wakati wa haja ndogo, haja ndogo ya mara kwa mara au haja ndogo kutoka kwa shida.


 


Chanzo Cha PID

Kuna bakteria wa aina nyingi wanaoweza kusababisha PID, lakini maambukizi ya gonorrhea na chlamydia ndiyo yanayoonekana zaidi. Bakteria hao huambukiza wakati tendo la ndoa linapofanyika bila ya kutumia kinga.


 



PID kusambaa kwa PID


Aghalabu, bakteria hawa huingia kwenye viungo ya uzazi vya mwanamke pale ulinzi wa kwenye shingo ya kizazi (cervix) unapovurugwa. Hii inaweza kutokea mathalani, wakati wa hedhi na baada ya kuzaa, mimba kuharibika au kutoa mimba. Mara chache bakteria huweza kujipenyeza wakati kifaa cho chote cha tiba kinapoingizwa kwenye nyumba ya uzazi.


Mazingira Hatarishi

Kuna vipengele ambavyo huweza kukuweka kwenye hatari kubwa zaidi ya kupata PID, navyo ni:


. Kuwa mwanamke uliye chini ya miaka 25 unayeshiriki ngono

. Kuwa na wapenzi zaidi ya mmoja

. Kuwa na mahusiano na mpenzi mwenye wapenzi zaidi ya mmoja

. Kufanya mapenzi bila kinga

. Kujisafisha na maji mara kwa mara

. Kuwa uliwahi kupata PID kabla au magonjwa mengine ya ngono


 


Madhara Yatokanayo Na PID

PID ambayo haikupata tiba inaweza kusababisha makovu na vifuko vyenye maji yenye wadudu kwenye mkondo wa njia ya uzazi ya mwanamke. Vitu hivi vinaweza kusababisha madhara ya kudumu kwenye viungo vya uzazi.


 


 


PID magonjwa


Madhara yanayoweza kutokea ni pamoja na:

. Mimba nje ya mirija (ectopic pregnancy). PID ndiyo sababu kubwa ya mimba kutunga nje ya kizazi. Mimba huweza kutunga nje ya kizazi endapo PID imesababisha makovu ndani ya mirija ya uzazi. Makovu haya husababisha yai lililopevushwa kushindwa kusafiri ndani ya mirija ya uzazi kuelekea kwenye nyumba ya uzazi. Badala yake yai hunata ndani ya mirija ya uzazi . Mimba nje ya kizazi husababisha utokaji wa damu usio wa kawaida unaoweza kukatisha maisha ya mwanamke.


. Ugumba. Uharibifu wa viungo vya uzazi huweza kusababisha ugumba – kushindwa kupata ujauzito. Kadiri unavyozidi kupata PID mara nyingi zaidi, ndivyo hatari ya ugumba inavyozidi. Kuchelewa kupata tiba ya PID kunaongeza hatari ya ugumba.


. Maumivu sugu ya nyonga. PID inaweza kusababisha maumivu ya nyonga yanayoweza kudumu kwa miaka mingi. Makovu ndani ya mirija ya uzazi na viungo vingine vya uzazi huweza kuleta maumivu wakati wa kujamiiana na wakati yai linadodondoshwa (ovulation).


. Tubo-ovarian abscess. PID huweza kusababisha kutunga kwa usaha na kufanya majipu ndani ya njia ya uzazi. Mara nyingi majibu haya hutokea ndani ya mirija ya uzazi na ovari, ingawa huweza kuota ndani ya nyumba ya uzazi na shingo ya kizazi. Kama tiba haitatolewa, unaweza kupata maambukizo hatarishi kwa maisha.


Tiba Ya PID

Tiba ya mara moja kwa kutumia dawa itaondoa maambukizo yaliyosababisha PID. Lakini, hakuna njia ya kukarabati makovu au uharibifu kwenye njia ya viungo vya uzazi uliotokana na PID. Tiba ya PID yaweza kuwa:


. Antibiotics. Daktari atakuandikia dawa inayoendana na chanzo cha tatizo lako. Utasubiri siku kama tatu kuona kama dawa ulizopewa zinafanya kazi.


. Kumtibu Mwezi wako. Kuzuia maambukizi, yafaa mwezi wako afanyiwe uchunguzi na atibiwe.


. Kuacha kushiriki ngono kwa muda. Acha kushiriki ngono hadi utakapomaliza tiba na kuona kuwa umepona.

. Kumtibu Mwezi wako. Kuzuia maambukizi, yafaa mwezi wako afanyiwe uchunguzi na atibiwe.


. Kuacha kushiriki ngono kwa muda. Acha kushiriki ngono hadi utakapomaliza tiba na kuona kuwa umepona.


ATHARI ZA PID


⚫ Ugumba kwa wanawake


⚫ Kupata Kansa ya shingo ya Uzazi.


⚫ Kutunga mimba nje ya kizazi kutokana na yai kushindwa kufika katika mji wa mimba kutokana na madhara ya PID katika mirija ya Uzazi.


⚫ KUSABABISHA majeraha nje na ndani ya mirija ya uzazi na hii hupelekea kuziba kwa mirija ya Uzazi.


⚫ Maumivu ya tumbo /ngonga mara kwa mara baada ya tendo la ndoa na kipindi cha uchavushwaji mayai (Ovulation).


JINSI YA KUEPUKA/KUJIKINGA NA PID


⚫ Epuka kuvaliana nguo za ndani.


⚫ Kuwa na tabia ya kupima mara kwa mara mfumo wako wa Uzazi.


⚫ Kuwa msafi wa mwili na nguo zako za ndan 


⚫ Kula lishe bora.


⚫ Epuka kufanya tendo la ndoa na mwenza wako mara baada ya kugundua ana magonjwa ya kujamiiana (STDs)



Tumia dawa Asili iitwayo UROGETIX 5 kwa matibabu ya haraka na uhakika ya PID.



TIBA NA USHAURI WASILIANA NASI

0755162724


Dr.Liwaya


Tiba Asili

Tanzania

Comments

Popular posts from this blog

DAWA YA KUTIBU JINO UKIWA NYUMBANI

DAWA YA KUTIBU MENO KWA HARAKA NA UHAKIKA Dawa hii imeniponesha mm mwenyewe nilikuwa nasumbuliwa na jino la juu na ndipo nilipoamua kuandaa dawa hii na imenitibu kwa HARAKA na ufanisi wa Hall ya juu sana na bado sijapatapo kuona dawa nzuri kama hii,huna haja ya kung'oa meno yako baada ya kuifahamu dawa hii eti kwasababu yanauma Mahitaji 1.✍ Mafuta ya karafuu/clove oil. 2.✍ mafuta ya Nazi/coconut oil. 3.✍ Kitunguu maji. 4.✍ Kitunguu swaum. 5.✍ Pilipili manga. 6.Chumvi ya mawe/unga wake MAANDALIZI Ponda ponda Kitunguu maji,Kitunguu swaumu,chumvi ya mawe na pilipili manga kisha changanya na mafuta na Nazi na mafuta ya karafuu kwa kiasi kidogo (robo kijiko kidogo cha chai) kisha chukua mchanganyiko huu kisha uweke juani kwa muda wa dakika 15 kisha toa juani MATUMIZI 1.ikiwa jino lina tundu chukua uji uji wa mchanganyiko huu kisha weka katika tundu na mafuta yake yapakaae pembezoni mwa jino linalouma. 2.ikiwa jina halina tundu pakaa mafuta ya mchanganyiko huu pembezoni kulizunguka jino...

TATIZO LA KUFUNGA CHOO NA KUPATA CHOO KIGUMU

Tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu ni jambo tunalolikwepa kwenye mazungumzo yetu ya kila siku. Hata hivyo ni tatizo kubwa katika jamii na mbaya zaidi wengi hawajuwi madhara yake ni nini ya kuendelea kulivumilia tatizo hili. Kupata choo kigumu au kufunga choo ni ishara ya tatizo lingine baya zaidi mwilini. Kama kuna jambo unapaswa uliepuke kwa nguvu zote basi ni hili. Kwa afya bora kabisa hakikisha unapata choo kila siku mara 2 hata mara 3. Choo kilaini siyo kigumu na chenye maumivu. Wakati mwingine utakapopata tatizo hili naomba usiwe na aibu kulisema wazi hata kwa boss wako ili upate matibabu kwa haraka. Kufunga choo au kupata choo kigumu ndiyo CHANZO KIKUU CHA UGONJWA WA BAWASIRI kwa waTanzania wengi na hii inachangiwa kwa sehemu kubwa kwa kula ugali wa sembe na kutokunywa maji mengi kila siku. Pamoja na hayo, hakuna ugonjwa rahisi kutibika kama huu ikiwa utaamua kushughulisha kichwa chako kidogo hasa kwa kuangalia unakula na kunywa nini kila siku. Inatakiwa ifahamike kuwa ...

NI KWA NAMNA GANI BACTERIA (H.pyori) Husababisha vidonda vya TUMBO

-Bacteria, Helicobacter pylori/Campilobacter pylori_* anaweza kusafiri kutoka kwa mtu Mmoja kwenda kwa mwingine kupitia njia zifuatazo: ⤵⤵⤵ (a).📎Kupitia mate (kunyonyana midomo) (b).📎Kupitia matapishi. (c).📎 Kupitia kinyesi (d).📎Kupitia chakula ama maji yaliyokuwa na bacteria hawa. SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA MTU KUAMBUKIZWA BACTERIA HAWA_ (H.pylori) ⚫ Kuishi mazingira yenye mikusanyiko mkubwa wa watu bila kuchukua tahadhar. ⚫ Kunywa maji yasiyokuwa safi. ⚫ Kula vyakula visivyooshwa mfano matunda na Mboga za majani. ⚫ Kuishi karibu na mtu mwenye vidonda vya tumbo bila kuchukua tahadhar. H.pylori anapoingia katika mwili wa binadamu huathiri uzio mwenye kulinda ukuta wa tumbo na utumbo mdogo (protective mucous) hali hii hupelekea kudhoofika kwa kuta katika tumbo na utumbo mdogo. Ukuta huu unapodhoofika husababisha Tindikali (Asidi) inayozalishwa tumbo kuunguza na kuuchimba ukuta wa tumbo pia Bacteria hawa huchimba ukuta wa tumbo na KUSABABISHA kutokea vidonda katika ukuta wa tumbo...