Skip to main content

VIDONDA VYA TUMBO,CHANZO,DALILI,NA TIBA ASILI YA VIDONDA VYA TUMBO

 VIDONDA VYA TUMBO,CHANZO,DALILI,NA TIBA ASILI YA VIDONDA VYA TUMBO


VIDONDA VYA TUMBO (PEPTICOL POWDER








  FIG1;DAWA ASILI YA VIDONDA VYA TUMBO



VIDONDA VYA TUMBO (PEPTIC ULCERS)


Ni vidonda vilivyo wazi ambavyo hutokea katika kuta za tumbo,sehemu ya juu ya utumbo mdogo au kwenye kuta za koromeo kutokana na bacteria waitwao H.pylori na asid inayozalishwa kwenye kuta za tumbo.


Vidonda vya tumbo vinatibika kirahisi ila vikicheleweshwa bila kutibiwa huweza kusababisha tatizo kubwa. Ni tatizo linalotesa sana na kuwanyima raha watu wengi, linahitaji umakini na pia husababisha magonjwa mengine kama kansa, amoeba (amiba), homa, kupungua uzito. nk


 


 AINA YA VIDONDA VYA TUMBO.


Kuna aina tatu ya vidonda vya tumbo


* GASTRIC ULCERS


  Hivi ni vidonda ambavyo hutokea ndani ya tumbo,kwenye kuta za tumbo.


* ESOPHAGEAL ULCERS


Hivi ni vidonda ambavyo hutokea ndani ya koo la chakula,kwenye kuta za koo la chakula.


* DUODENAL ULCERS


Ni vidonda ambavyo katika sehemu ya juu ya utumbo mdogo uitwao duodenum








Peptic ulcers in the stomach and duodenum


FIG2;PEPTIC ULCERS


 


 


CHANZO CHA VIDONDA VYA TUMBO


 


Vidonda vya tumbo vina vyanzo tofauti ili vyote ni vile vinavyohusiana na mmeng’enyo, vyanzo hivyo ni;


Ø Bakteria waitwao Helicobacter pylori (H. pylori)

Ø Matumizi ya mara kwa mara ya dawa za kupunguza maumivu kama asprin(bayer), (NSAIDs), (Advil, Aleve, na zingine)

Ø Msongo mawazo (stress)

Ø Kula vyakula vinavyozalisha acid kwa wingi

Ø Kunywa pombe na vinywaji vikali kupitiliza.

Ø Uvutaji wa sigara.

Ø Kuto kula mlo kwa mpangilio maalumu

Ø Kansa ya tumbo

   


DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO

Dalili za vidonda vya tumbo hujitokeza baada ya kula au kabla ya kula, ila mara nyingi wengi huwa wanazipuuzia na kuendelea kukuza tatizo, vidonda vya tumbo vina dalili kama;


Ø Kupata maumivu ya tumbo ya kuwaka moto (kuunguza) baada na kabla ya kula

Ø Kupatwa na kiungulia(heartburn) karibu na chembe ya moyo

Ø Tumbo kujaa gesi na kuvimbiwa

Ø Kichefuchefu na kutapika tena yawezekana kutapika damu

Ø Kupata haja kubwa ya rangi ya kahawia au nyeusi cheenye harufu mbaya sana, pia haja yaweza kuchanganyikana na damu

Ø Kupoteza hamu ya kula na kupungua uzito

Ø Kushindwa kupumua vizuri

 


JINSI YA KUEPUKANA NA VIDONDA VYA TUMBO


Ø Kunywa maji mengi

Ø Punguza mawazo, fanya mazoezi yatakupunguza na mawazo

Ø Punguza (balance) kiwango cha lehemu (choresterol) mwilini

Ø Usivute sigara

Ø Punguza au acha kunywa pombe

Ø Kula vizuri vyakula bora hasa asilia na sio vyakula vyenye kemikali

Ø Lala vizuri kwa muda mzuri – masaa 7 hadi 9

 


Tatizo la Vidonda vya tumbo linatibika kufuatana na mda wa tatizo, mara nyingi wagonjwa wamekuwa wakizalau dalili za vidonda vya tumbo na kudhani kuwa hakuna madhara makubwa.


 


MATIBABU


Kwa matatizo ya vidonda vya tumbo,watu wengi wamekuwa hakihangaika sana kupata matibabu sahihi na badala yake wamekuwa wakitumia dawa za kutuliza matatizo ya vidonda vya tumbo na si kutibu tatizo moja kwa moja.


Zipo dawa asili ambazo hutibu matatizo ya vidonda vya tumbo kwa haraka sana na tiba ya kudumu,mfano kuna dawa ya asili iitwayo PEPTICOL POWDER,dawa hii hutibu kwa haraka sana matatizo ya vidonda vya tumbo.


 


Kwa mahitaji ya dawa ya kutibu matatizo ya vidonda vya tumbo kwa haraka na kudumu,wasiliana nami kwa;


 


Dr.Liwaya

Tiba asili, Tanzania

Whatsap; +255 755 162 724

Calls; +255 755 162 724

Email; muhammadliwaya@gmail.com 

Comments

Popular posts from this blog

NI KWA NAMNA GANI BACTERIA (H.pyori) Husababisha vidonda vya TUMBO

-Bacteria, Helicobacter pylori/Campilobacter pylori_* anaweza kusafiri kutoka kwa mtu Mmoja kwenda kwa mwingine kupitia njia zifuatazo: ⤵⤵⤵ (a).📎Kupitia mate (kunyonyana midomo) (b).📎Kupitia matapishi. (c).📎 Kupitia kinyesi (d).📎Kupitia chakula ama maji yaliyokuwa na bacteria hawa. SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA MTU KUAMBUKIZWA BACTERIA HAWA_ (H.pylori) ⚫ Kuishi mazingira yenye mikusanyiko mkubwa wa watu bila kuchukua tahadhar. ⚫ Kunywa maji yasiyokuwa safi. ⚫ Kula vyakula visivyooshwa mfano matunda na Mboga za majani. ⚫ Kuishi karibu na mtu mwenye vidonda vya tumbo bila kuchukua tahadhar. H.pylori anapoingia katika mwili wa binadamu huathiri uzio mwenye kulinda ukuta wa tumbo na utumbo mdogo (protective mucous) hali hii hupelekea kudhoofika kwa kuta katika tumbo na utumbo mdogo. Ukuta huu unapodhoofika husababisha Tindikali (Asidi) inayozalishwa tumbo kuunguza na kuuchimba ukuta wa tumbo pia Bacteria hawa huchimba ukuta wa tumbo na KUSABABISHA kutokea vidonda katika ukuta wa tumbo...

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, CHANZO, DALILI NA TIBA YAKE ASILIA

Ufafanuzi wa jumla wa tatizo la nguvu za kiume na tiba yake​ Kuishiwa nguvu za kiume ni jambo la kawaida kwa wanaume wengi. Ni kushindwa kwa uume kudumu kusimama barabara kwa ajili ya tendo la ndoa, au kuwahi kufika kileleni. Tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume huongezeka siku had I siku. Tafiti mbalimbali zinasema wanaume wengi wenye umri kuanzia miaka 35 na kuendelea ndio wanaosumbuliwa na tatizo hili kwa kiasi kikubwa. Wanaume wenye elimu ndogo juu ya utendaji kazi wa mwili na afya ndio wanaokabiliwa sana na tatizo hili. Hii ni kutokana na kwamba wengi wao wanakuwa hawaelewi aina ya vyakula vinavyoongeza nguvu za kiume na za mwili kwa ujumla, namna wanavyotakiwa kuishi ili kupunguza janga hilo, wanakunywa pombe na hawajishughulishi na mazoezi ya viungo. Mazoezi ya viungo hupunguza tatizo la kuishiwa nguvu za kiume kwa asilimia kubwa sana. Kupungukiwa nguvu za kiume kunaweza pia kuwa kumetokana na mambo ya kihisia, kwa kiingereza ‘emotional causes’. Vitu vingine vinavyoweza kusababi...

TATIZO LA KUFUNGA CHOO NA KUPATA CHOO KIGUMU

Tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu ni jambo tunalolikwepa kwenye mazungumzo yetu ya kila siku. Hata hivyo ni tatizo kubwa katika jamii na mbaya zaidi wengi hawajuwi madhara yake ni nini ya kuendelea kulivumilia tatizo hili. Kupata choo kigumu au kufunga choo ni ishara ya tatizo lingine baya zaidi mwilini. Kama kuna jambo unapaswa uliepuke kwa nguvu zote basi ni hili. Kwa afya bora kabisa hakikisha unapata choo kila siku mara 2 hata mara 3. Choo kilaini siyo kigumu na chenye maumivu. Wakati mwingine utakapopata tatizo hili naomba usiwe na aibu kulisema wazi hata kwa boss wako ili upate matibabu kwa haraka. Kufunga choo au kupata choo kigumu ndiyo CHANZO KIKUU CHA UGONJWA WA BAWASIRI kwa waTanzania wengi na hii inachangiwa kwa sehemu kubwa kwa kula ugali wa sembe na kutokunywa maji mengi kila siku. Pamoja na hayo, hakuna ugonjwa rahisi kutibika kama huu ikiwa utaamua kushughulisha kichwa chako kidogo hasa kwa kuangalia unakula na kunywa nini kila siku. Inatakiwa ifahamike kuwa ...