Skip to main content

UGONJWA WA KISUKARI,CHANZO CHAKE,DALILI ZAKE,ATHARI NA MATIBABU YAKE ASILI

Ugonjwa wa Kisukari ni hali ya Kiwango cha Sukari kuzidi kwenye damu kutokana na tezi za kongosho kushindwa kuzalisha vichocheo vya kutosha vya insulin, au mwili kupoteza sifa na uwezo wa kuvitumia vichocheo vya insulin vyenye kazi ya kudhibiti kiwango cha Sukari mwilini.




=====

Kisukari ni ugonjwa unaoambatana na hali ya uwepo wa sukari nyingi kupita kiasi kwenye damu.

Hutokea baada ya tezi za kongosho kushindwa kuzalisha vichocheo vya kutosha vya insulin, au mwili ukipoteza sifa na uwezo wa kuvitumia vichocheo vya insulin vinavyo zalishwa hivyo kufanya ongezeko kubwa la sukari litokee kuliko kiwango cha kawaida kinachotakiwa.

625AAC9D-EB21-46CD-BDB0-C220A74A40D8.jpeg

Insulin ndiyo vichocheo vinavyotumiwa na mwili katika kudhibiti ongezeko la sukari.

Aina Zake
Kuna aina nyingi za kisukari, lakini wataalam hupenda kuugawa ugonjwa huu kwenye aina kuu tatu ambazo ni kisukari aina ya kwanza, kisukari aina ya pili pamoja na kisukari cha ujauzito.
Aina ya kwanza ya kisukari hutokea baada ya mwili kukosa sifa na uwezo wa kuzalisha vichocheo vya insulin. Mara nyingi husababishwa na mwili wenyewe kuzishambulia seli zinazozalisha vichocheo hivi. Walau asilimia 10 ya wagonjwa wote wa kisukari huwa wapo kwenye kundi hili. Hufahamika pia kama kisukari kinachotegemea insulin
Aina ya pili ya kisukari hutokea kwa watu ambao miili yao huzalisha vichocheo vya insulin, lakini huwa sugu kiasi cha kushindwa kuvitumia kikamilifu katika kudhibiti sukari. Walau asilimia 90 ya wagonjwa wote wa kisukari huwa wapo kwenye kundi hili. Hufahamika pia kama Kisukari kisichotegemea insulini
Kisukari cha ujauzito hutokea wakati wa ujauzito pekee. Husababishwa na baadhi ya vichocheo ambavyo mwili wa mwanamke huvitengeneza ili kumlinda mtoto. Aina hii ya kisukari mara nyingi huisha baada ya kujifungua

Vihatarishi
Baadhi ya mambo huongeza nafasi ya kuugua ugonjwa wa kisukari. Miongoni mwake ni-
Kutoka kwenye familia yenye historia ya uwepo wa ugonjwa huu
Kuwa na uzito mkubwa
Umri wa zaidi ya miaka 45
Kutokufanya kazi yoyote au mazoezi yanayoongeza utimamu wa mwili
Kuwa na shinikizo kubwa la damu na mafuta mengi
Kuwa na ujauzito
Uwepo wa changamoto kwenye mfumo wa taarifa za mfumo wa kinga za mwili unaoweza kushambulia tezi za kongosho
Kuwa mvutaji wa sigara
Dalili
Dalili za kisukari husababishwa na uwepo wa sukari nyingi mwilini ambazo huufanya mwili uanze kuonesha tabia hasi. Baadhi ya dalili hizo ni
Kuhisi njaa kila mara
Ganzi, kuchomwachomwa au kutohisi unapoguswa sehemu za miguu, viganja na vidole.
Kujisaidia haja ndogo mara kwa mara
Kuhisi kiu mara kwa mara
Kupungua uzito wa mwili na kukonda
Kupatwa na vidonda visivyo pona kirahisi
Kuwa dhaifu, kukosa nguvu na kujisikia mchovu kila wakati
Kupungua kwa uwezo wa macho katika kuona
Kupungua kwa hamu na uwezo wa mwanamme kwenye kushiriki tendo la ndoa
Maambukizi ya mara kwa mara ya mfumo wa mkojo, miwasho sehemu za siri na fangasi wa mara kwa mara

Athari
Kisukari ni mojawapo ya magonjwa yanayo ongoza kwa kuua watu wengi duniani kila mwaka pamoja na kusababisha ulemavu na utegemezi wa kudumu.

Pia, huchangia kwa kiasi kikubwa upofu, magonjwa ya moyo, maambukizi makali mwilini yanayoweza kusababisha vidonda visivyopona, maumivu ya kudumu ya miguu, ugonjwa wa figo, kiharusi, kudumaa kwa afya ya uzazi kwa jinsia zote, kujifungua kabla ya wakati pamoja na kifafa cha ujauzito.

Kati ya mwaka 2000 – 2016, kulikuwa na ongezeko la asilimia 5 la vifo vya mapema duniani vilivyo sababishwa na kisukari.

Mwaka 2019, ugonjwa wa kisukari ulishika namba 9 duniani katika kusababisha vifo ambapo takriban watu 1.5 M walipoteza maisha kutokana na ugonjwa huu.

Matibabu na Ushauri
Matibabu ya kisukari huhusisha mazoezi, lishe, kudhibiti uzito pamoja na matumizi ya dawa.




Kutokana na aina husika ya kisukari, mhudumu wa afya atatoa dawa pamoja na ushauri wa namna bora ya kutumia dawa hizo. Mfano wa dawa hizo ni Metformin, glibenclamide, insulin n.k
Shiriki mazoezi, husaidia kuunguza nishati pamoja na kupunguza usugu wa mwili katika kutumia vichocheo vya insulin.
Lishe huchukua sehemu kubwa ya matibabu kwa kuwa karibia kila chakula hugeuzwa kuwa sukari mwilini. Uchaguzi wa vyakula vyenye kiasi kidogo cha mafuta na wanga, nafaka nzima, nyuzi lishe nyingi, matunda pamoja na mboga za majani hushauriwa.
Ni muhimu kudhibiti ongezeko la uzito wa mwili. Ukubwa wa athari za kisukari mara nyingi huenda sambamba na kiasi cha uzito alio nao mgonjwa.
Usivute sigara
Punguza matumizi ya pombe
Punguza matumizi ya chumvi hadi kijiko kimoja kwa siku

Kisukari ni ugonjwa wenye kutibika kwa dawa za asili hasa pale utakapobahatika kupata dawa ya uhakika katika kutibu kisukari mfano wa dawa za uhakika zenye kuondosha kabsa kisukari ni dawa ya asili iitwayo DM POWDER 

Wasiliana na mimi kwa maelezo zaidi

0755162724
Dr Liwaya

Dar es salaam, Ilala 

Comments

Popular posts from this blog

ZIJUE FAIDA,MADHARA YA KITUNGUU SWAUMU KATIKA MWILI WA BINADAMU

MAGONJWA YANAYOTIBIKA KUPITIA KITUNGUU SAUMU Huyeyusha mafuta mwilini (kolestro) Husafisha njia ya mkojo na kutibu U.T.I Hutibu amoeba, minyoo na Bakteria wengine Huzuia kuhara damu (Dysentery) Huondoa Gesi tumboni Hutibu msokoto wa tumbo Hutibu Typhoid Huondoa mabaka mabaka kwenye ngozi Hutibu mafua na malaria Hutibu kifua kikuu (ukitumia kitunguu swaumu kesho yake unaweza kutokwa na makohozi mengi tu ambayo ni ishara kwamba kweli kinatibu kifua kikuu (TB) Hutibu kipindupindu Hutibu upele Huvunjavunja mawe katika figo Hutibu mba kichwani Huupa nguvu ubongo. Kazi nzuri niliyopenda zaidi katika kitunguu swaumu. Huzuia meno kung’ooka na kutuliza maumivu Huongeza SANA nguvu za kiume pia hutibu uanithi (kushindwa kusimama kabisa uume) Hutibu maumivu ya kichwa Hutibu kizunguzungu Hutibu shinikizo la juu la damu Huzuia saratani/kansa Hutibu maumivu ya jongo/gout Huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula Huongeza hamu ya kula Huzuia damu kuganda Husaidia kutibu kisukari Husaidia kutibu ...

TATIZO LA KUFUNGA CHOO NA KUPATA CHOO KIGUMU

Tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu ni jambo tunalolikwepa kwenye mazungumzo yetu ya kila siku. Hata hivyo ni tatizo kubwa katika jamii na mbaya zaidi wengi hawajuwi madhara yake ni nini ya kuendelea kulivumilia tatizo hili. Kupata choo kigumu au kufunga choo ni ishara ya tatizo lingine baya zaidi mwilini. Kama kuna jambo unapaswa uliepuke kwa nguvu zote basi ni hili. Kwa afya bora kabisa hakikisha unapata choo kila siku mara 2 hata mara 3. Choo kilaini siyo kigumu na chenye maumivu. Wakati mwingine utakapopata tatizo hili naomba usiwe na aibu kulisema wazi hata kwa boss wako ili upate matibabu kwa haraka. Kufunga choo au kupata choo kigumu ndiyo CHANZO KIKUU CHA UGONJWA WA BAWASIRI kwa waTanzania wengi na hii inachangiwa kwa sehemu kubwa kwa kula ugali wa sembe na kutokunywa maji mengi kila siku. Pamoja na hayo, hakuna ugonjwa rahisi kutibika kama huu ikiwa utaamua kushughulisha kichwa chako kidogo hasa kwa kuangalia unakula na kunywa nini kila siku. Inatakiwa ifahamike kuwa ...

UGONJWA WA KIHARUSI, CHANZO, DALILI NA TIBA YAKE ASILIA.

Pengine umekuwa ukisikia sehemu mbalimbali kuhusu tatizo la kiharusi lakini bado hukuwahi kusoma na kuelewa vizuri. Karibu katika mfululizo wa makala zetu ambapo utajifunza nini maana ya kiharusi, aina za kiharusi, nini chanzo ama visababishi vyake. jinsi gani upunguze hatari ya kupata ugonjwa huu na huduma ya dawa za virutubisho ambavyo vitakusaidia kuondoa athari za tatizo. Maelezo Ya Utangulizi Kwa Tatizo La Stroke Kiharusi au stroke hutokea bila kutoa kiashiria chochote. Na ndio maana kuchukua tahadhari za kuepuka kutokea kwa tatizo ni muhimu zaidi. Kwasababu endapo utapata kiharusi na kwa bahati njema mwili ukaendela kufanya kazi basi matokeo na madhara yake yatakusumbua sana maisha yote. Kuepuka madhara makubwa ya kiharusi mgonjwa anahitajika kutibiwa ndani ya saa moja baada ya kupata shambulizi. Hakikisha pia unafika haraka hospitali kama ukigundua moja ya dalili zifuatazo zimekutokea bila kutaraji. Kushindwa ghafla kutembea na kupoteza balansi ya mwili. Kuchanganyikiwa ghafla n...