Skip to main content

UGONJWA WA KISUKARI,CHANZO CHAKE,DALILI ZAKE,ATHARI NA MATIBABU YAKE ASILI

Ugonjwa wa Kisukari ni hali ya Kiwango cha Sukari kuzidi kwenye damu kutokana na tezi za kongosho kushindwa kuzalisha vichocheo vya kutosha vya insulin, au mwili kupoteza sifa na uwezo wa kuvitumia vichocheo vya insulin vyenye kazi ya kudhibiti kiwango cha Sukari mwilini.




=====

Kisukari ni ugonjwa unaoambatana na hali ya uwepo wa sukari nyingi kupita kiasi kwenye damu.

Hutokea baada ya tezi za kongosho kushindwa kuzalisha vichocheo vya kutosha vya insulin, au mwili ukipoteza sifa na uwezo wa kuvitumia vichocheo vya insulin vinavyo zalishwa hivyo kufanya ongezeko kubwa la sukari litokee kuliko kiwango cha kawaida kinachotakiwa.

625AAC9D-EB21-46CD-BDB0-C220A74A40D8.jpeg

Insulin ndiyo vichocheo vinavyotumiwa na mwili katika kudhibiti ongezeko la sukari.

Aina Zake
Kuna aina nyingi za kisukari, lakini wataalam hupenda kuugawa ugonjwa huu kwenye aina kuu tatu ambazo ni kisukari aina ya kwanza, kisukari aina ya pili pamoja na kisukari cha ujauzito.
Aina ya kwanza ya kisukari hutokea baada ya mwili kukosa sifa na uwezo wa kuzalisha vichocheo vya insulin. Mara nyingi husababishwa na mwili wenyewe kuzishambulia seli zinazozalisha vichocheo hivi. Walau asilimia 10 ya wagonjwa wote wa kisukari huwa wapo kwenye kundi hili. Hufahamika pia kama kisukari kinachotegemea insulin
Aina ya pili ya kisukari hutokea kwa watu ambao miili yao huzalisha vichocheo vya insulin, lakini huwa sugu kiasi cha kushindwa kuvitumia kikamilifu katika kudhibiti sukari. Walau asilimia 90 ya wagonjwa wote wa kisukari huwa wapo kwenye kundi hili. Hufahamika pia kama Kisukari kisichotegemea insulini
Kisukari cha ujauzito hutokea wakati wa ujauzito pekee. Husababishwa na baadhi ya vichocheo ambavyo mwili wa mwanamke huvitengeneza ili kumlinda mtoto. Aina hii ya kisukari mara nyingi huisha baada ya kujifungua

Vihatarishi
Baadhi ya mambo huongeza nafasi ya kuugua ugonjwa wa kisukari. Miongoni mwake ni-
Kutoka kwenye familia yenye historia ya uwepo wa ugonjwa huu
Kuwa na uzito mkubwa
Umri wa zaidi ya miaka 45
Kutokufanya kazi yoyote au mazoezi yanayoongeza utimamu wa mwili
Kuwa na shinikizo kubwa la damu na mafuta mengi
Kuwa na ujauzito
Uwepo wa changamoto kwenye mfumo wa taarifa za mfumo wa kinga za mwili unaoweza kushambulia tezi za kongosho
Kuwa mvutaji wa sigara
Dalili
Dalili za kisukari husababishwa na uwepo wa sukari nyingi mwilini ambazo huufanya mwili uanze kuonesha tabia hasi. Baadhi ya dalili hizo ni
Kuhisi njaa kila mara
Ganzi, kuchomwachomwa au kutohisi unapoguswa sehemu za miguu, viganja na vidole.
Kujisaidia haja ndogo mara kwa mara
Kuhisi kiu mara kwa mara
Kupungua uzito wa mwili na kukonda
Kupatwa na vidonda visivyo pona kirahisi
Kuwa dhaifu, kukosa nguvu na kujisikia mchovu kila wakati
Kupungua kwa uwezo wa macho katika kuona
Kupungua kwa hamu na uwezo wa mwanamme kwenye kushiriki tendo la ndoa
Maambukizi ya mara kwa mara ya mfumo wa mkojo, miwasho sehemu za siri na fangasi wa mara kwa mara

Athari
Kisukari ni mojawapo ya magonjwa yanayo ongoza kwa kuua watu wengi duniani kila mwaka pamoja na kusababisha ulemavu na utegemezi wa kudumu.

Pia, huchangia kwa kiasi kikubwa upofu, magonjwa ya moyo, maambukizi makali mwilini yanayoweza kusababisha vidonda visivyopona, maumivu ya kudumu ya miguu, ugonjwa wa figo, kiharusi, kudumaa kwa afya ya uzazi kwa jinsia zote, kujifungua kabla ya wakati pamoja na kifafa cha ujauzito.

Kati ya mwaka 2000 – 2016, kulikuwa na ongezeko la asilimia 5 la vifo vya mapema duniani vilivyo sababishwa na kisukari.

Mwaka 2019, ugonjwa wa kisukari ulishika namba 9 duniani katika kusababisha vifo ambapo takriban watu 1.5 M walipoteza maisha kutokana na ugonjwa huu.

Matibabu na Ushauri
Matibabu ya kisukari huhusisha mazoezi, lishe, kudhibiti uzito pamoja na matumizi ya dawa.




Kutokana na aina husika ya kisukari, mhudumu wa afya atatoa dawa pamoja na ushauri wa namna bora ya kutumia dawa hizo. Mfano wa dawa hizo ni Metformin, glibenclamide, insulin n.k
Shiriki mazoezi, husaidia kuunguza nishati pamoja na kupunguza usugu wa mwili katika kutumia vichocheo vya insulin.
Lishe huchukua sehemu kubwa ya matibabu kwa kuwa karibia kila chakula hugeuzwa kuwa sukari mwilini. Uchaguzi wa vyakula vyenye kiasi kidogo cha mafuta na wanga, nafaka nzima, nyuzi lishe nyingi, matunda pamoja na mboga za majani hushauriwa.
Ni muhimu kudhibiti ongezeko la uzito wa mwili. Ukubwa wa athari za kisukari mara nyingi huenda sambamba na kiasi cha uzito alio nao mgonjwa.
Usivute sigara
Punguza matumizi ya pombe
Punguza matumizi ya chumvi hadi kijiko kimoja kwa siku

Kisukari ni ugonjwa wenye kutibika kwa dawa za asili hasa pale utakapobahatika kupata dawa ya uhakika katika kutibu kisukari mfano wa dawa za uhakika zenye kuondosha kabsa kisukari ni dawa ya asili iitwayo DM POWDER 

Wasiliana na mimi kwa maelezo zaidi

0755162724
Dr Liwaya

Dar es salaam, Ilala 

Comments

Popular posts from this blog

NI KWA NAMNA GANI BACTERIA (H.pyori) Husababisha vidonda vya TUMBO

-Bacteria, Helicobacter pylori/Campilobacter pylori_* anaweza kusafiri kutoka kwa mtu Mmoja kwenda kwa mwingine kupitia njia zifuatazo: ⤵⤵⤵ (a).📎Kupitia mate (kunyonyana midomo) (b).📎Kupitia matapishi. (c).📎 Kupitia kinyesi (d).📎Kupitia chakula ama maji yaliyokuwa na bacteria hawa. SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA MTU KUAMBUKIZWA BACTERIA HAWA_ (H.pylori) ⚫ Kuishi mazingira yenye mikusanyiko mkubwa wa watu bila kuchukua tahadhar. ⚫ Kunywa maji yasiyokuwa safi. ⚫ Kula vyakula visivyooshwa mfano matunda na Mboga za majani. ⚫ Kuishi karibu na mtu mwenye vidonda vya tumbo bila kuchukua tahadhar. H.pylori anapoingia katika mwili wa binadamu huathiri uzio mwenye kulinda ukuta wa tumbo na utumbo mdogo (protective mucous) hali hii hupelekea kudhoofika kwa kuta katika tumbo na utumbo mdogo. Ukuta huu unapodhoofika husababisha Tindikali (Asidi) inayozalishwa tumbo kuunguza na kuuchimba ukuta wa tumbo pia Bacteria hawa huchimba ukuta wa tumbo na KUSABABISHA kutokea vidonda katika ukuta wa tumbo...

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, CHANZO, DALILI NA TIBA YAKE ASILIA

Ufafanuzi wa jumla wa tatizo la nguvu za kiume na tiba yake​ Kuishiwa nguvu za kiume ni jambo la kawaida kwa wanaume wengi. Ni kushindwa kwa uume kudumu kusimama barabara kwa ajili ya tendo la ndoa, au kuwahi kufika kileleni. Tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume huongezeka siku had I siku. Tafiti mbalimbali zinasema wanaume wengi wenye umri kuanzia miaka 35 na kuendelea ndio wanaosumbuliwa na tatizo hili kwa kiasi kikubwa. Wanaume wenye elimu ndogo juu ya utendaji kazi wa mwili na afya ndio wanaokabiliwa sana na tatizo hili. Hii ni kutokana na kwamba wengi wao wanakuwa hawaelewi aina ya vyakula vinavyoongeza nguvu za kiume na za mwili kwa ujumla, namna wanavyotakiwa kuishi ili kupunguza janga hilo, wanakunywa pombe na hawajishughulishi na mazoezi ya viungo. Mazoezi ya viungo hupunguza tatizo la kuishiwa nguvu za kiume kwa asilimia kubwa sana. Kupungukiwa nguvu za kiume kunaweza pia kuwa kumetokana na mambo ya kihisia, kwa kiingereza ‘emotional causes’. Vitu vingine vinavyoweza kusababi...

DAWA YA KUTIBU JINO UKIWA NYUMBANI

DAWA YA KUTIBU MENO KWA HARAKA NA UHAKIKA Dawa hii imeniponesha mm mwenyewe nilikuwa nasumbuliwa na jino la juu na ndipo nilipoamua kuandaa dawa hii na imenitibu kwa HARAKA na ufanisi wa Hall ya juu sana na bado sijapatapo kuona dawa nzuri kama hii,huna haja ya kung'oa meno yako baada ya kuifahamu dawa hii eti kwasababu yanauma Mahitaji 1.✍ Mafuta ya karafuu/clove oil. 2.✍ mafuta ya Nazi/coconut oil. 3.✍ Kitunguu maji. 4.✍ Kitunguu swaum. 5.✍ Pilipili manga. 6.Chumvi ya mawe/unga wake MAANDALIZI Ponda ponda Kitunguu maji,Kitunguu swaumu,chumvi ya mawe na pilipili manga kisha changanya na mafuta na Nazi na mafuta ya karafuu kwa kiasi kidogo (robo kijiko kidogo cha chai) kisha chukua mchanganyiko huu kisha uweke juani kwa muda wa dakika 15 kisha toa juani MATUMIZI 1.ikiwa jino lina tundu chukua uji uji wa mchanganyiko huu kisha weka katika tundu na mafuta yake yapakaae pembezoni mwa jino linalouma. 2.ikiwa jina halina tundu pakaa mafuta ya mchanganyiko huu pembezoni kulizunguka jino...