Skip to main content

TATIZO LA MAWE KWENYE MFUKO WA NYONGO

JINSI YA KUDHIBITI TATIZO LA MAWE KWENYE MFUKO WA NYONGO


Kabla ya kulifahamu tatizo la mawe kwenye mfuko wa nyongo,hebu kwanza fahamu kwa ufupi nyongo ni nini na kazi yake ni ipi. Si hivyo tu bali pia nataka ufahamu mfuko wa nyongo ni nini na una kazi gani ndipo ufahamu jinsi mawe yanavyotokea kwenye mfuko wa nyongo.

NYONGO( BILE) NI NINI?

Nyongo ni juisi inayotumika kumeng'enyea chakula ambayo huzalishwa na ini na kutunzwa ndani ya mfuko wa nyongo. Nyongo haina kimeng'enya (enzymes) lakini ina asidi inayosaidia kumeng'enya mchanganyiko wa mafuta mwilini.

KAZI ZA NYONGO

Nyongo ina kazi kubwa mbili:
Kusaidia umeng'enywaji wa mafuta na kusharabiwa kwenye utumbo mwembamba-Chumvi chumvi iliyo kwenye nyongo hujishikiza na mafuta yanayotokana na chakula na kupenya kuingia kwenye mishipa ya damu na badaye hurejeshwa kwenye nyongo.

Kusaidia kutoa uchafu nje toka kwenye damu- Mwili una kawaida ya kuvunja chembe hai nyekundu za damu zilizozeeka na kutengeneza mpya. Nyongo ndio huchua mabaki haya (bilirubin) na kutoa ncje kama uchafu.

MFUKO WA NYONGO (GALLBLADDER) NI KITU GANI?


Mfuko wa nyongo ni kifuko kidogo sana kama ukubwa wa pera hivi ambacho hutunza nyongo. Kama nilivyoeleza hapo juu,nyongo inayotunzwa kwenye mfuko wa nyongo huzalishwa na ini. Ini huzalisha ml 600 hadi lita moja ya nyongo kwa siku (masaa 24) japo mfuko wa nyongo huweza kutunza ml 40 hadi 60 tu za nyongo kwa mara moja.

MAWE KWENYE MFUKO WA NYONGO-GALLSTONE

Mawe kwenye mfuko wa nyongo ni miongoni mwa matatizo yenye kuisumbua sana jamii kwa sasa. Ukisikia mawe kwenye mfuko wa nyongo ni vizuri ukafahamu kuwa si mawe halisi bali ni vichembe chembe vigumu hivi vinavyokusanya kwenye kiasi kikubwa hutunzwa kwenye mfuko wa nyongo.

AINA ZA MAWE KWENYE MFUKO WA NYONGO

Ziko aina mbili za mawe kwenye mfuko wa nyongo. Aina hizo hutokana na jinsi mawe hayo yanavyosababishwa

Cholestrol Stones- ni mawe kwenye mfuko wa nyongo yanayosababishwa na kuzidi kwa lehemu (cholestrol) kwenye mfuko wa nyongo. Mawe haya huwa na rangi ya kjani-njano hivi. Ndiyo aina iliyoenea na kuzoeleka sana ya mawe kwenye mfuko wa nyongo.

Pigment Stones- Ni mawe kwenye mfuko wa nyongo yanayotokana na kujikusanya kwa bilirubin (mabaki ya kuvunjwa vunjwa kwa chembe hai nyekundu za damu) kwenye mfuko wa nyongo.

CHANZO CHA MAWE KWENYE MFUKO WA NYONGO

Ziko sababu kuu tatu zinazochangia mawe kujaa kwenye mfuko wa nyongo. Sababu hizo ni kama zifuatazo:

1. Kuongezeka lehemu (cholestrol) kwenye nyongo: kwa kawaida nyongo huzaishwa na ini na kutunzwa ndani ya mfuko wa nyongo. Lakini pia ini huzalisha lehemu japo kuna kiasi fulani cha lehemu huingia mwilini kwa njia ya chakula. Lehemu ikizidi kwenye nyongo husababisha mawe kutokea.

2. Nyongo kujawa na bilirubin nyingi- bilirubin ni mabaki yanayotokana na kuvunjwa vunjwa kwa chembe hai nyekundu za damu (red blood cells) ndani ya ini. Mabaki haya yasipotolewa mwilini hujikusanya na kujazana kwenye mfuko wa nyongo.

3. Nyongo kubakia kwenye mfuko wa nyongo-unapomaliza kula chakula kwa kawaida nyongo yote hutoka na kwenda kusaidia katika umeng'enywaji wa chakula. Kama itatokea mfuko wa nyongo kuachia nyongo kidogo na nyingine kubakia kwa muda mrefu,basi tatizo la mawe ndani ya mfuko wa nyongo hutokea.

DALILI NA MADHARA YA GALLSTONES

Japo zaidi ya 80% ya wagonjwa wa gallstone hukosa kupata dalili,wachache huweza kukutwa na dalili zafuatayo:

Maumivu makali upande kulia juu ya tumbo

-Kucheua na miungurumo ndani ya tumbo baaada ya kula

-Kutapika mara kwa mara

-Maumivu makali upande wa bega la kulia
Kutokwa jasho kwa wingi

-Maumivu makali ya mgongo katikati ya mabega

Madhara Ya Gallstone ni kama yafuatayo:

-Kuziba mirija ya nyongo

-Maambukizi kwenye mfuko wa nyongo

-Mrija wa kongosho kuziba

-Manjano

-Kansa ya mfuko wa nyongo

TIBA YA MGONJWA MWENYE MAWE KWENYE MFUKO WA NYONGO

Ili tiba ya mgonjwa mwenye gallstone iwe na ufanisi,ni lazima sababu zinazosababisha mawe kutokea zifahamike. Kuepuka cholestrol nyingi kujikusanya kwenye mfuko wa nyongo na kuondoa bilirubin iliyogandamana kwenye mfuko wa nyongo husaidia kwa kiwango kikubwa kuondoa tatizo hili. Matatizo yote yanayosababisha mawe kutokea husababishwa na matatizo ya ini. Matatizo ya ini kama vile ini kuharibika (liver cirrhosis),ini kuwa na mafuta (fatty liver),homa ya ini (hepatits B,C na D) huweza kusababisha mawe kutokea
Dawa zetu za kuondoa mawe kwenye mfuko wa nyongo zitakusaidi kuimarisha ini na utendaji kazi wake,kuondoa vyanzo vya mawe kwenye mfuko wa nyongo yaani lehemu,bilirubin na kufungua mirija ya nyongo. Lakini pia utatakiwa kupata virutubishi vya kuimarisha na kujenga ini kwa kuwa hufanya kazi nyingi sana mwilini,zaidi ya kazi mia tano.

Wengi waliotumia dawa hizi kwa ajili ya kuondoa mawe kwenye mfuko wa nyongo,waliahirisha kupata upasuaji,na hawajalalamika tena kuumwa tumbo ama kupata dalili tena ila tu walipokwenda kupima walijikuta mawe hayapo tena na wanaendelea vizuri hadi sasa.

Kama una tatizo hili,ni wakati wako mwafaka kutumia tiba hizi ili kupata ufumbuzi wa tatizo lako.

JINSI YA KUDHIBITI MAWE KWENYE MFUKO WA NYONGO

-Kula chakula chenye afya kama vile mboga za majani,matunda na nafaka nzima.

-Kunywa maji mengi kila siku hata kama huna kiu

-Epuka uzito kupita kiasi,jitahidi kuwa na uzito unaoendana na urefu wako.

-Epuka kula vyakula vyenye mafuta mengi kwa wingi

-Epuka kukonda

-Epuka kutumia vidonge vya uzazi wa mpango
-Kula vyakula vyenye nyuzi nyuzi kwa wingi

-Tunza ini lako kuepuka lisidhurike na kuharibika.

Hebu chukua mda wako kutafakari juu ya ugonjwa huu huku ukichukua hatua ya kutibu tatizo hili kwa ajili ya kulinda afya yako


Asante sana na kwa muda wako, naomba niishie hapa. Nikaribishe Kama una Maswali, Karibuni Sana..


Je, Unahitaji Kupata Huduma Kutoka Liwaya Herbal Clinic ? Basi wasiliana nasi Kwa namba hizi: 0755162724



Pia Unaweza kutembelea tovuti yetu: www.liwayaherbalclinic.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

NI KWA NAMNA GANI BACTERIA (H.pyori) Husababisha vidonda vya TUMBO

-Bacteria, Helicobacter pylori/Campilobacter pylori_* anaweza kusafiri kutoka kwa mtu Mmoja kwenda kwa mwingine kupitia njia zifuatazo: ⤵⤵⤵ (a).📎Kupitia mate (kunyonyana midomo) (b).📎Kupitia matapishi. (c).📎 Kupitia kinyesi (d).📎Kupitia chakula ama maji yaliyokuwa na bacteria hawa. SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA MTU KUAMBUKIZWA BACTERIA HAWA_ (H.pylori) ⚫ Kuishi mazingira yenye mikusanyiko mkubwa wa watu bila kuchukua tahadhar. ⚫ Kunywa maji yasiyokuwa safi. ⚫ Kula vyakula visivyooshwa mfano matunda na Mboga za majani. ⚫ Kuishi karibu na mtu mwenye vidonda vya tumbo bila kuchukua tahadhar. H.pylori anapoingia katika mwili wa binadamu huathiri uzio mwenye kulinda ukuta wa tumbo na utumbo mdogo (protective mucous) hali hii hupelekea kudhoofika kwa kuta katika tumbo na utumbo mdogo. Ukuta huu unapodhoofika husababisha Tindikali (Asidi) inayozalishwa tumbo kuunguza na kuuchimba ukuta wa tumbo pia Bacteria hawa huchimba ukuta wa tumbo na KUSABABISHA kutokea vidonda katika ukuta wa tumbo...

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, CHANZO, DALILI NA TIBA YAKE ASILIA

Ufafanuzi wa jumla wa tatizo la nguvu za kiume na tiba yake​ Kuishiwa nguvu za kiume ni jambo la kawaida kwa wanaume wengi. Ni kushindwa kwa uume kudumu kusimama barabara kwa ajili ya tendo la ndoa, au kuwahi kufika kileleni. Tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume huongezeka siku had I siku. Tafiti mbalimbali zinasema wanaume wengi wenye umri kuanzia miaka 35 na kuendelea ndio wanaosumbuliwa na tatizo hili kwa kiasi kikubwa. Wanaume wenye elimu ndogo juu ya utendaji kazi wa mwili na afya ndio wanaokabiliwa sana na tatizo hili. Hii ni kutokana na kwamba wengi wao wanakuwa hawaelewi aina ya vyakula vinavyoongeza nguvu za kiume na za mwili kwa ujumla, namna wanavyotakiwa kuishi ili kupunguza janga hilo, wanakunywa pombe na hawajishughulishi na mazoezi ya viungo. Mazoezi ya viungo hupunguza tatizo la kuishiwa nguvu za kiume kwa asilimia kubwa sana. Kupungukiwa nguvu za kiume kunaweza pia kuwa kumetokana na mambo ya kihisia, kwa kiingereza ‘emotional causes’. Vitu vingine vinavyoweza kusababi...

DAWA YA KUTIBU JINO UKIWA NYUMBANI

DAWA YA KUTIBU MENO KWA HARAKA NA UHAKIKA Dawa hii imeniponesha mm mwenyewe nilikuwa nasumbuliwa na jino la juu na ndipo nilipoamua kuandaa dawa hii na imenitibu kwa HARAKA na ufanisi wa Hall ya juu sana na bado sijapatapo kuona dawa nzuri kama hii,huna haja ya kung'oa meno yako baada ya kuifahamu dawa hii eti kwasababu yanauma Mahitaji 1.✍ Mafuta ya karafuu/clove oil. 2.✍ mafuta ya Nazi/coconut oil. 3.✍ Kitunguu maji. 4.✍ Kitunguu swaum. 5.✍ Pilipili manga. 6.Chumvi ya mawe/unga wake MAANDALIZI Ponda ponda Kitunguu maji,Kitunguu swaumu,chumvi ya mawe na pilipili manga kisha changanya na mafuta na Nazi na mafuta ya karafuu kwa kiasi kidogo (robo kijiko kidogo cha chai) kisha chukua mchanganyiko huu kisha uweke juani kwa muda wa dakika 15 kisha toa juani MATUMIZI 1.ikiwa jino lina tundu chukua uji uji wa mchanganyiko huu kisha weka katika tundu na mafuta yake yapakaae pembezoni mwa jino linalouma. 2.ikiwa jina halina tundu pakaa mafuta ya mchanganyiko huu pembezoni kulizunguka jino...