Skip to main content

TATIZO LA KUKOMA KWA HEDHI

Nini Maana Ya Kukoma Hedhi?
 




Kukoma hedhi ni hali ya kawaida ambayo wanawake wote huipitia umri ukiwa mkubwa. Neno kukoma hedhi linaweza likaelezea mabadiliko yo yote yanayomtokea mwanamke muda mfupi kabla au baada ya kuacha kupata siku zake, ikiwa ni ishara ya mwisho wa kuzaa.



Nini Kinasababisha Kukoma hedhi?
 

Mwanamke huzaliwa akiwa na idadi kamili ya mayai, ambayo hutunzwa ndani ya ovari. Ovari hizi pia hutengeneza homoni za estrogen na progesterone, ambazo husimamia hedhi na upevushwaji wa mayai. Kukoma hedhi maana yake ovari kukoma kuachia yai kila mwezi na kusimama kuingia mwezini.

Kukoma hedhi ni sehemu ya kawaida ya mwili kuzeeka na hutokea baada ya kufikia umri wa mika 40. Lakini baadhi ya wanawake wanawake wanaweza kukoma hedhi mapema zaidi, ikiwa ni matokeo ya upasuaji, kama hysterectomy, au uharibifu kwenye ovari, kama baada ya tiba ya chemotherapy. Kukoma hedhi kabla ya miaka 40, kwa sababu yo yote ile huitwa premature menopause.



Dalili Za Kukoma Hedhi
 

Wanawake wengi wanaokaribia kukoma hedhi wanapata hot flashes, yaani ghafla kusika joto linalosambaa sehemu ya juu ya mwili, vikiambatana na hali ya kutahayari na kutokwa jasho. Hali hii huwa si kali sana kwa wanawake wengi lakini kwa wengine huwa mbaya.


Dalili nyingine zinazotokea mwanamke anapokaribia kukoma hedhi ni pamoja na:

  1. Hedhi zisizo na mpangilio au zinazorukaruka
  2. Kukosa usingizi
  3. Kusikia hasira mara kwa mara
  4. Uchovu
  5. Mfadhaiko
  6. Moyo kwenda mbio
  7. Maumivu ya kichwa
  8. Maumivu ya joints na misuli
  9. Mabadiliko katika kusikia hamu ya tendo la ndoa
  10. Uyabisi wa uke
  11. Shida kudhibiti haja ndogo

Si wanawake wote wanaopata dalili hizi zote.


KUKOMA KWA HEDHI KUNAANZA UMRI GANI? 

Wanawake wengi huanza kupata dalili za kukoma kwa hedhi kati ya umri wa miaka 45 hadi 55 lakini katika hali isiyo ya kawaida wengine wanaweza kupata hata kabla ya kutimiza umri wa miaka 40.

Shirika hilo hata hivyo linasema si rahisi kutabiri ni lini mwanamke atafikia ukomo wa hedhi ijapokuwa kuna uhusiano kati ya umri na vigezo kama vile afya na jenetiki.

Takwimu zinaonesha kuwa idadi ya wanawake wanaofikia ukomo wa hedhi inaongezeka ambapo mwaka 2021 wanawake wenye umri wa miaka 50 na kuendelea walikuwa asilimia 26 ya wanawake na wasichana wote duniani kote.

Idadi hiyo ni sawa na ongezeko kwa asilimia 22 ikilinganishwa na miaka 10 iliyopita.

Halikadhalika wanawake wanaishi muda mrefu zaidi ambapo mwanamke aliyekuwa na umri wa miaka 60 mwaka 2019 anatarajiwa kuishi kwa wastani wa miaka mingine 21.


Usikose kuuliza maswali wakati wo wote kuhusiana na mada zetu, tutafurahi sana kuona kuwa tumekujibu vyema.

 

Kwa maswali zaidi na ushauri piga 0755 162 724

Au bonyeza link ya WhatsApp ipo mwisho upande wa kulia wa makala hii.

Comments

Popular posts from this blog

NI KWA NAMNA GANI BACTERIA (H.pyori) Husababisha vidonda vya TUMBO

-Bacteria, Helicobacter pylori/Campilobacter pylori_* anaweza kusafiri kutoka kwa mtu Mmoja kwenda kwa mwingine kupitia njia zifuatazo: ⤵⤵⤵ (a).📎Kupitia mate (kunyonyana midomo) (b).📎Kupitia matapishi. (c).📎 Kupitia kinyesi (d).📎Kupitia chakula ama maji yaliyokuwa na bacteria hawa. SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA MTU KUAMBUKIZWA BACTERIA HAWA_ (H.pylori) ⚫ Kuishi mazingira yenye mikusanyiko mkubwa wa watu bila kuchukua tahadhar. ⚫ Kunywa maji yasiyokuwa safi. ⚫ Kula vyakula visivyooshwa mfano matunda na Mboga za majani. ⚫ Kuishi karibu na mtu mwenye vidonda vya tumbo bila kuchukua tahadhar. H.pylori anapoingia katika mwili wa binadamu huathiri uzio mwenye kulinda ukuta wa tumbo na utumbo mdogo (protective mucous) hali hii hupelekea kudhoofika kwa kuta katika tumbo na utumbo mdogo. Ukuta huu unapodhoofika husababisha Tindikali (Asidi) inayozalishwa tumbo kuunguza na kuuchimba ukuta wa tumbo pia Bacteria hawa huchimba ukuta wa tumbo na KUSABABISHA kutokea vidonda katika ukuta wa tumbo...

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, CHANZO, DALILI NA TIBA YAKE ASILIA

Ufafanuzi wa jumla wa tatizo la nguvu za kiume na tiba yake​ Kuishiwa nguvu za kiume ni jambo la kawaida kwa wanaume wengi. Ni kushindwa kwa uume kudumu kusimama barabara kwa ajili ya tendo la ndoa, au kuwahi kufika kileleni. Tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume huongezeka siku had I siku. Tafiti mbalimbali zinasema wanaume wengi wenye umri kuanzia miaka 35 na kuendelea ndio wanaosumbuliwa na tatizo hili kwa kiasi kikubwa. Wanaume wenye elimu ndogo juu ya utendaji kazi wa mwili na afya ndio wanaokabiliwa sana na tatizo hili. Hii ni kutokana na kwamba wengi wao wanakuwa hawaelewi aina ya vyakula vinavyoongeza nguvu za kiume na za mwili kwa ujumla, namna wanavyotakiwa kuishi ili kupunguza janga hilo, wanakunywa pombe na hawajishughulishi na mazoezi ya viungo. Mazoezi ya viungo hupunguza tatizo la kuishiwa nguvu za kiume kwa asilimia kubwa sana. Kupungukiwa nguvu za kiume kunaweza pia kuwa kumetokana na mambo ya kihisia, kwa kiingereza ‘emotional causes’. Vitu vingine vinavyoweza kusababi...

DAWA YA KUTIBU JINO UKIWA NYUMBANI

DAWA YA KUTIBU MENO KWA HARAKA NA UHAKIKA Dawa hii imeniponesha mm mwenyewe nilikuwa nasumbuliwa na jino la juu na ndipo nilipoamua kuandaa dawa hii na imenitibu kwa HARAKA na ufanisi wa Hall ya juu sana na bado sijapatapo kuona dawa nzuri kama hii,huna haja ya kung'oa meno yako baada ya kuifahamu dawa hii eti kwasababu yanauma Mahitaji 1.✍ Mafuta ya karafuu/clove oil. 2.✍ mafuta ya Nazi/coconut oil. 3.✍ Kitunguu maji. 4.✍ Kitunguu swaum. 5.✍ Pilipili manga. 6.Chumvi ya mawe/unga wake MAANDALIZI Ponda ponda Kitunguu maji,Kitunguu swaumu,chumvi ya mawe na pilipili manga kisha changanya na mafuta na Nazi na mafuta ya karafuu kwa kiasi kidogo (robo kijiko kidogo cha chai) kisha chukua mchanganyiko huu kisha uweke juani kwa muda wa dakika 15 kisha toa juani MATUMIZI 1.ikiwa jino lina tundu chukua uji uji wa mchanganyiko huu kisha weka katika tundu na mafuta yake yapakaae pembezoni mwa jino linalouma. 2.ikiwa jina halina tundu pakaa mafuta ya mchanganyiko huu pembezoni kulizunguka jino...