Skip to main content

TATIZO LA KUKOMA KWA HEDHI

Nini Maana Ya Kukoma Hedhi?
 




Kukoma hedhi ni hali ya kawaida ambayo wanawake wote huipitia umri ukiwa mkubwa. Neno kukoma hedhi linaweza likaelezea mabadiliko yo yote yanayomtokea mwanamke muda mfupi kabla au baada ya kuacha kupata siku zake, ikiwa ni ishara ya mwisho wa kuzaa.



Nini Kinasababisha Kukoma hedhi?
 

Mwanamke huzaliwa akiwa na idadi kamili ya mayai, ambayo hutunzwa ndani ya ovari. Ovari hizi pia hutengeneza homoni za estrogen na progesterone, ambazo husimamia hedhi na upevushwaji wa mayai. Kukoma hedhi maana yake ovari kukoma kuachia yai kila mwezi na kusimama kuingia mwezini.

Kukoma hedhi ni sehemu ya kawaida ya mwili kuzeeka na hutokea baada ya kufikia umri wa mika 40. Lakini baadhi ya wanawake wanawake wanaweza kukoma hedhi mapema zaidi, ikiwa ni matokeo ya upasuaji, kama hysterectomy, au uharibifu kwenye ovari, kama baada ya tiba ya chemotherapy. Kukoma hedhi kabla ya miaka 40, kwa sababu yo yote ile huitwa premature menopause.



Dalili Za Kukoma Hedhi
 

Wanawake wengi wanaokaribia kukoma hedhi wanapata hot flashes, yaani ghafla kusika joto linalosambaa sehemu ya juu ya mwili, vikiambatana na hali ya kutahayari na kutokwa jasho. Hali hii huwa si kali sana kwa wanawake wengi lakini kwa wengine huwa mbaya.


Dalili nyingine zinazotokea mwanamke anapokaribia kukoma hedhi ni pamoja na:

  1. Hedhi zisizo na mpangilio au zinazorukaruka
  2. Kukosa usingizi
  3. Kusikia hasira mara kwa mara
  4. Uchovu
  5. Mfadhaiko
  6. Moyo kwenda mbio
  7. Maumivu ya kichwa
  8. Maumivu ya joints na misuli
  9. Mabadiliko katika kusikia hamu ya tendo la ndoa
  10. Uyabisi wa uke
  11. Shida kudhibiti haja ndogo

Si wanawake wote wanaopata dalili hizi zote.


KUKOMA KWA HEDHI KUNAANZA UMRI GANI? 

Wanawake wengi huanza kupata dalili za kukoma kwa hedhi kati ya umri wa miaka 45 hadi 55 lakini katika hali isiyo ya kawaida wengine wanaweza kupata hata kabla ya kutimiza umri wa miaka 40.

Shirika hilo hata hivyo linasema si rahisi kutabiri ni lini mwanamke atafikia ukomo wa hedhi ijapokuwa kuna uhusiano kati ya umri na vigezo kama vile afya na jenetiki.

Takwimu zinaonesha kuwa idadi ya wanawake wanaofikia ukomo wa hedhi inaongezeka ambapo mwaka 2021 wanawake wenye umri wa miaka 50 na kuendelea walikuwa asilimia 26 ya wanawake na wasichana wote duniani kote.

Idadi hiyo ni sawa na ongezeko kwa asilimia 22 ikilinganishwa na miaka 10 iliyopita.

Halikadhalika wanawake wanaishi muda mrefu zaidi ambapo mwanamke aliyekuwa na umri wa miaka 60 mwaka 2019 anatarajiwa kuishi kwa wastani wa miaka mingine 21.


Usikose kuuliza maswali wakati wo wote kuhusiana na mada zetu, tutafurahi sana kuona kuwa tumekujibu vyema.

 

Kwa maswali zaidi na ushauri piga 0755 162 724

Au bonyeza link ya WhatsApp ipo mwisho upande wa kulia wa makala hii.

Comments

Popular posts from this blog

DAWA YA KUTIBU JINO UKIWA NYUMBANI

DAWA YA KUTIBU MENO KWA HARAKA NA UHAKIKA Dawa hii imeniponesha mm mwenyewe nilikuwa nasumbuliwa na jino la juu na ndipo nilipoamua kuandaa dawa hii na imenitibu kwa HARAKA na ufanisi wa Hall ya juu sana na bado sijapatapo kuona dawa nzuri kama hii,huna haja ya kung'oa meno yako baada ya kuifahamu dawa hii eti kwasababu yanauma Mahitaji 1.✍ Mafuta ya karafuu/clove oil. 2.✍ mafuta ya Nazi/coconut oil. 3.✍ Kitunguu maji. 4.✍ Kitunguu swaum. 5.✍ Pilipili manga. 6.Chumvi ya mawe/unga wake MAANDALIZI Ponda ponda Kitunguu maji,Kitunguu swaumu,chumvi ya mawe na pilipili manga kisha changanya na mafuta na Nazi na mafuta ya karafuu kwa kiasi kidogo (robo kijiko kidogo cha chai) kisha chukua mchanganyiko huu kisha uweke juani kwa muda wa dakika 15 kisha toa juani MATUMIZI 1.ikiwa jino lina tundu chukua uji uji wa mchanganyiko huu kisha weka katika tundu na mafuta yake yapakaae pembezoni mwa jino linalouma. 2.ikiwa jina halina tundu pakaa mafuta ya mchanganyiko huu pembezoni kulizunguka jino...

TATIZO LA KUFUNGA CHOO NA KUPATA CHOO KIGUMU

Tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu ni jambo tunalolikwepa kwenye mazungumzo yetu ya kila siku. Hata hivyo ni tatizo kubwa katika jamii na mbaya zaidi wengi hawajuwi madhara yake ni nini ya kuendelea kulivumilia tatizo hili. Kupata choo kigumu au kufunga choo ni ishara ya tatizo lingine baya zaidi mwilini. Kama kuna jambo unapaswa uliepuke kwa nguvu zote basi ni hili. Kwa afya bora kabisa hakikisha unapata choo kila siku mara 2 hata mara 3. Choo kilaini siyo kigumu na chenye maumivu. Wakati mwingine utakapopata tatizo hili naomba usiwe na aibu kulisema wazi hata kwa boss wako ili upate matibabu kwa haraka. Kufunga choo au kupata choo kigumu ndiyo CHANZO KIKUU CHA UGONJWA WA BAWASIRI kwa waTanzania wengi na hii inachangiwa kwa sehemu kubwa kwa kula ugali wa sembe na kutokunywa maji mengi kila siku. Pamoja na hayo, hakuna ugonjwa rahisi kutibika kama huu ikiwa utaamua kushughulisha kichwa chako kidogo hasa kwa kuangalia unakula na kunywa nini kila siku. Inatakiwa ifahamike kuwa ...

NI KWA NAMNA GANI BACTERIA (H.pyori) Husababisha vidonda vya TUMBO

-Bacteria, Helicobacter pylori/Campilobacter pylori_* anaweza kusafiri kutoka kwa mtu Mmoja kwenda kwa mwingine kupitia njia zifuatazo: ⤵⤵⤵ (a).📎Kupitia mate (kunyonyana midomo) (b).📎Kupitia matapishi. (c).📎 Kupitia kinyesi (d).📎Kupitia chakula ama maji yaliyokuwa na bacteria hawa. SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA MTU KUAMBUKIZWA BACTERIA HAWA_ (H.pylori) ⚫ Kuishi mazingira yenye mikusanyiko mkubwa wa watu bila kuchukua tahadhar. ⚫ Kunywa maji yasiyokuwa safi. ⚫ Kula vyakula visivyooshwa mfano matunda na Mboga za majani. ⚫ Kuishi karibu na mtu mwenye vidonda vya tumbo bila kuchukua tahadhar. H.pylori anapoingia katika mwili wa binadamu huathiri uzio mwenye kulinda ukuta wa tumbo na utumbo mdogo (protective mucous) hali hii hupelekea kudhoofika kwa kuta katika tumbo na utumbo mdogo. Ukuta huu unapodhoofika husababisha Tindikali (Asidi) inayozalishwa tumbo kuunguza na kuuchimba ukuta wa tumbo pia Bacteria hawa huchimba ukuta wa tumbo na KUSABABISHA kutokea vidonda katika ukuta wa tumbo...