Skip to main content

VYAKULA AMBAVYO NI VIZURI SANA KWENYE KUSAIDIA NA KUIMARISHA MFUMO WA UZAZI WA MWANAUME

 VYAKULA AMBAVYO NI VIZURI SANA KWENYE KUSAIDIA NA KUIMARISHA MFUMO WA UZAZI WA MWANAUME




NAFAKA

●Nafaka husaidia katika kuzalisha homoni za testosterone, pia huwezesha mtu kuwa na nguvu tele hatimaye kuongeza nguvu zake za kiume kutokana na virutubisho mwili unavyopata. 


▪︎Vyakula vya nafaka vimesheheni nishati nyingi, nafaka zina nyuzinyuzi (fibres) na sukari

ambazo kusaidia kutunza uzito wa mwili.


▪︎Kula nafaka zisizokobolewa kama vile brown bread badala ya white bread, pia kula nafaka halisi

badala ya cornflakes ni jambo zuri kiafya zina saidia kutokupa mwili wa mafuta mengi, 


▪︎ikumbukwe uwepo wa mafuta mabaya yana athiri mishipa ya damu ikiwamo ya uume.



TANGAWIZI

●Tangawizi ni aina ya kiungo mizizi ambacho husisimua sana mfumo wa mzunguko wa damu mwilini. 

▪︎Mzunguko unapokuwa mzuri huwezesha damu kwenda sehemu za viungo vya uzazi ikiwamo uume. 


▪︎Tangawizi imekuwa ikitumika sana maeneo ya Asia kwa ajili ya wanaume wenye tatizo la nguvu

za kiume. 


▪︎Pia baadhi ya Viungo ambavyo viko katika pilau ni mojawapo ya vitu ambavyo miaka na miaka imetumika

maeneo ya Asia na Amerika ya Kaskazini kama viungo vyakula vinavyoimarisha nguvu za kiume.



KOMAMANGA

●Komamanga (Pemigranate) ni aina ya matunda yenye rangi nyekundu na mwonekano kama apple. 


●Tunda hili husaidia kuamsha mishipa ya fahamu na kuweka mawasiliano sahihi ya mwili na hivyo kumwongezea mtu uwezo kwa kufanya tendo la ndoa kwa hamasa kubwa. 


●Hivyo humfanya mtumiaji kupokea hisia za mapenzi kwa urahisi zaidi.



*MBEGU MBALI MBALI ZA MATUNDA, IKIWEMO TIKITIMAJI NA MBEGU ZA MABOGA*

●Mchanganyiko wa mbegu mbalimbali za matunda ikiwamo tikiti maji na mbegu za maboga husaidia

kuondoa ACID mwilini na kuupa mwili virutubisho tele vinavyoimarisha afya ya uzazi wa mwanaume na kumfanya mtu awe mwenye afya njema.



ASALI

●Asali Ina madini yanayoitwa boron ambayo husaidia mwili kutumia homoni. 


●Hata vitabu vya dini hueleza ulaji wa asali na masega yake kama mlo wenye kuupa mwili nguvu. 


•Pia Zipo tafititi lukuki kuhusu faida za asali, faida mojawapo ikiwamo  kusaisia kuongeza nguvu za kiume.



KARANGA

●Karanga.

-Huhusika moja kwa moja na kutunza mfumo wa mzunguko wa damu kuwa na afya. Husaidia

kuimarisha mzunguko wa damu katika maeneo ya uzazi 


▪︎hivyo kuongeza msisimko wa tendo.

▪︎Pia karanga zina madini muhimu kama vile madini ya magineziamu, tindikali ya foliki na madini ya zinki ambayo ni muhimu sana katika uzalishaji wa mbegu za mwanaume na kuongeza hisia.



BLUEBERRY

●Blueberry ni matunda yanayosaidia sana kuongeza nguvu za kiume, wengi hupendelea kuyaita "viagra asilia" kutokana na kazi inayoifanya mwilini. 


●Blueberries ina virutubishi vinavyoimarisha mishipa ya damu na kusaidia mzunguko mzuri wa damu mwilini.

▪︎ Damu ndio kila kitu katika nguvu

za kiume. 


▪︎Vilevile, blueberries zina nyuzinyuzi ambazo husaidia kuondoa kolesteroli

(Cholestrol) mwilini kabla haijanganda kwenye mishipa ya damu. 


▪︎Kuwa na mzunguko mzuri wa

damu husaidia mwanaume aweze kuhimiri tendo la ndoa kwa muda mrefu zaidi.



MTINI (FIGS)

●Mtini (Figs) ni matunda yenye kiwango kikubwa cha amino asidi, ambayo ni kiungo kikubwa katika

kuzalisha homoni mwilini. 


●Homoni ndio kishawishi cha nguvu za kiume mwilini. 


●Kukosa amino asidi huweza kusababisha kukosa hamu ya mapenzi au kupungukiwa na nguvu za kiume.



VITUNGUU SAUMU

●Vitunguu saumu vina allicin, kiambato kinachosaidia mzunguko mzuri wa damu kwenye viungo

vya uzazi. 


●Kuwa na mzunguko mzuri wa damu kwenye uume ni sababu kubwa ya kuongeza stamina katika tendo la ndoa.



NDIZI

●Kuwa na stamina ni muhimu katika ufanyaji mapenzi. 


●Ndizi ni chanzo kikubwa cha vitamin B ambayo husaidia sana katika kuongeza stamina na nguvu mwilini hasa wakati wa kufanya kazi nzito. 


●Ndizi ina kimeng’enyo cha Bromelain ambacho huongeza nguvu za kiume, ashki ya mapenzi

(libido).



MIZIZI YA MACA

●Maca Root Ni mmea maarufu sana huko Brazil ambao umekua ukitumiwa na wanaume na wanawake wengi ili kuwapa nguvu ya muda mrefu,kuondoa stress,afya ya uzazi,kubalance hormone,na kuwapa

hamu ya tendo la ndoa,n.k

N.k....

●Binafsi ninashauri kutumia njia asilia katika kutatua matatizo yako yote ya kiafya. Mwili una njia

zake za kurekebisha kila kitu. 


▪︎Ukiona kuna tatizo inaashiria kuna upungufu ambao unatakiwa

kurekebishwa. 


▪︎Kutumia madawa makali hudhoosha mwili na hivyo kuupunguzia uwezo wa

kufanya kazi kama inavyotakiwa. 


▪︎Ni vizuri kama utamuona daktari kama ukiona hakuna

kinachowezekana kabla hujaanza kutumia madawa.



📌Mara nyingi njia asilia hutumia muda mrefu kuleta mabadiliko, lakini matokeo yake hudumu zaidi kuliko kutumia madawa makali ambayo hu-BOOST na hayatibu.


Dr Liwaya

0755162724

Comments

Popular posts from this blog

DAWA YA KUTIBU JINO UKIWA NYUMBANI

DAWA YA KUTIBU MENO KWA HARAKA NA UHAKIKA Dawa hii imeniponesha mm mwenyewe nilikuwa nasumbuliwa na jino la juu na ndipo nilipoamua kuandaa dawa hii na imenitibu kwa HARAKA na ufanisi wa Hall ya juu sana na bado sijapatapo kuona dawa nzuri kama hii,huna haja ya kung'oa meno yako baada ya kuifahamu dawa hii eti kwasababu yanauma Mahitaji 1.✍ Mafuta ya karafuu/clove oil. 2.✍ mafuta ya Nazi/coconut oil. 3.✍ Kitunguu maji. 4.✍ Kitunguu swaum. 5.✍ Pilipili manga. 6.Chumvi ya mawe/unga wake MAANDALIZI Ponda ponda Kitunguu maji,Kitunguu swaumu,chumvi ya mawe na pilipili manga kisha changanya na mafuta na Nazi na mafuta ya karafuu kwa kiasi kidogo (robo kijiko kidogo cha chai) kisha chukua mchanganyiko huu kisha uweke juani kwa muda wa dakika 15 kisha toa juani MATUMIZI 1.ikiwa jino lina tundu chukua uji uji wa mchanganyiko huu kisha weka katika tundu na mafuta yake yapakaae pembezoni mwa jino linalouma. 2.ikiwa jina halina tundu pakaa mafuta ya mchanganyiko huu pembezoni kulizunguka jino...

TATIZO LA KUFUNGA CHOO NA KUPATA CHOO KIGUMU

Tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu ni jambo tunalolikwepa kwenye mazungumzo yetu ya kila siku. Hata hivyo ni tatizo kubwa katika jamii na mbaya zaidi wengi hawajuwi madhara yake ni nini ya kuendelea kulivumilia tatizo hili. Kupata choo kigumu au kufunga choo ni ishara ya tatizo lingine baya zaidi mwilini. Kama kuna jambo unapaswa uliepuke kwa nguvu zote basi ni hili. Kwa afya bora kabisa hakikisha unapata choo kila siku mara 2 hata mara 3. Choo kilaini siyo kigumu na chenye maumivu. Wakati mwingine utakapopata tatizo hili naomba usiwe na aibu kulisema wazi hata kwa boss wako ili upate matibabu kwa haraka. Kufunga choo au kupata choo kigumu ndiyo CHANZO KIKUU CHA UGONJWA WA BAWASIRI kwa waTanzania wengi na hii inachangiwa kwa sehemu kubwa kwa kula ugali wa sembe na kutokunywa maji mengi kila siku. Pamoja na hayo, hakuna ugonjwa rahisi kutibika kama huu ikiwa utaamua kushughulisha kichwa chako kidogo hasa kwa kuangalia unakula na kunywa nini kila siku. Inatakiwa ifahamike kuwa ...

NI KWA NAMNA GANI BACTERIA (H.pyori) Husababisha vidonda vya TUMBO

-Bacteria, Helicobacter pylori/Campilobacter pylori_* anaweza kusafiri kutoka kwa mtu Mmoja kwenda kwa mwingine kupitia njia zifuatazo: ⤵⤵⤵ (a).📎Kupitia mate (kunyonyana midomo) (b).📎Kupitia matapishi. (c).📎 Kupitia kinyesi (d).📎Kupitia chakula ama maji yaliyokuwa na bacteria hawa. SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA MTU KUAMBUKIZWA BACTERIA HAWA_ (H.pylori) ⚫ Kuishi mazingira yenye mikusanyiko mkubwa wa watu bila kuchukua tahadhar. ⚫ Kunywa maji yasiyokuwa safi. ⚫ Kula vyakula visivyooshwa mfano matunda na Mboga za majani. ⚫ Kuishi karibu na mtu mwenye vidonda vya tumbo bila kuchukua tahadhar. H.pylori anapoingia katika mwili wa binadamu huathiri uzio mwenye kulinda ukuta wa tumbo na utumbo mdogo (protective mucous) hali hii hupelekea kudhoofika kwa kuta katika tumbo na utumbo mdogo. Ukuta huu unapodhoofika husababisha Tindikali (Asidi) inayozalishwa tumbo kuunguza na kuuchimba ukuta wa tumbo pia Bacteria hawa huchimba ukuta wa tumbo na KUSABABISHA kutokea vidonda katika ukuta wa tumbo...