Skip to main content

VYAKULA AMBAVYO NI VIZURI SANA KWENYE KUSAIDIA NA KUIMARISHA MFUMO WA UZAZI WA MWANAUME

 VYAKULA AMBAVYO NI VIZURI SANA KWENYE KUSAIDIA NA KUIMARISHA MFUMO WA UZAZI WA MWANAUME




NAFAKA

●Nafaka husaidia katika kuzalisha homoni za testosterone, pia huwezesha mtu kuwa na nguvu tele hatimaye kuongeza nguvu zake za kiume kutokana na virutubisho mwili unavyopata. 


▪︎Vyakula vya nafaka vimesheheni nishati nyingi, nafaka zina nyuzinyuzi (fibres) na sukari

ambazo kusaidia kutunza uzito wa mwili.


▪︎Kula nafaka zisizokobolewa kama vile brown bread badala ya white bread, pia kula nafaka halisi

badala ya cornflakes ni jambo zuri kiafya zina saidia kutokupa mwili wa mafuta mengi, 


▪︎ikumbukwe uwepo wa mafuta mabaya yana athiri mishipa ya damu ikiwamo ya uume.



TANGAWIZI

●Tangawizi ni aina ya kiungo mizizi ambacho husisimua sana mfumo wa mzunguko wa damu mwilini. 

▪︎Mzunguko unapokuwa mzuri huwezesha damu kwenda sehemu za viungo vya uzazi ikiwamo uume. 


▪︎Tangawizi imekuwa ikitumika sana maeneo ya Asia kwa ajili ya wanaume wenye tatizo la nguvu

za kiume. 


▪︎Pia baadhi ya Viungo ambavyo viko katika pilau ni mojawapo ya vitu ambavyo miaka na miaka imetumika

maeneo ya Asia na Amerika ya Kaskazini kama viungo vyakula vinavyoimarisha nguvu za kiume.



KOMAMANGA

●Komamanga (Pemigranate) ni aina ya matunda yenye rangi nyekundu na mwonekano kama apple. 


●Tunda hili husaidia kuamsha mishipa ya fahamu na kuweka mawasiliano sahihi ya mwili na hivyo kumwongezea mtu uwezo kwa kufanya tendo la ndoa kwa hamasa kubwa. 


●Hivyo humfanya mtumiaji kupokea hisia za mapenzi kwa urahisi zaidi.



*MBEGU MBALI MBALI ZA MATUNDA, IKIWEMO TIKITIMAJI NA MBEGU ZA MABOGA*

●Mchanganyiko wa mbegu mbalimbali za matunda ikiwamo tikiti maji na mbegu za maboga husaidia

kuondoa ACID mwilini na kuupa mwili virutubisho tele vinavyoimarisha afya ya uzazi wa mwanaume na kumfanya mtu awe mwenye afya njema.



ASALI

●Asali Ina madini yanayoitwa boron ambayo husaidia mwili kutumia homoni. 


●Hata vitabu vya dini hueleza ulaji wa asali na masega yake kama mlo wenye kuupa mwili nguvu. 


•Pia Zipo tafititi lukuki kuhusu faida za asali, faida mojawapo ikiwamo  kusaisia kuongeza nguvu za kiume.



KARANGA

●Karanga.

-Huhusika moja kwa moja na kutunza mfumo wa mzunguko wa damu kuwa na afya. Husaidia

kuimarisha mzunguko wa damu katika maeneo ya uzazi 


▪︎hivyo kuongeza msisimko wa tendo.

▪︎Pia karanga zina madini muhimu kama vile madini ya magineziamu, tindikali ya foliki na madini ya zinki ambayo ni muhimu sana katika uzalishaji wa mbegu za mwanaume na kuongeza hisia.



BLUEBERRY

●Blueberry ni matunda yanayosaidia sana kuongeza nguvu za kiume, wengi hupendelea kuyaita "viagra asilia" kutokana na kazi inayoifanya mwilini. 


●Blueberries ina virutubishi vinavyoimarisha mishipa ya damu na kusaidia mzunguko mzuri wa damu mwilini.

▪︎ Damu ndio kila kitu katika nguvu

za kiume. 


▪︎Vilevile, blueberries zina nyuzinyuzi ambazo husaidia kuondoa kolesteroli

(Cholestrol) mwilini kabla haijanganda kwenye mishipa ya damu. 


▪︎Kuwa na mzunguko mzuri wa

damu husaidia mwanaume aweze kuhimiri tendo la ndoa kwa muda mrefu zaidi.



MTINI (FIGS)

●Mtini (Figs) ni matunda yenye kiwango kikubwa cha amino asidi, ambayo ni kiungo kikubwa katika

kuzalisha homoni mwilini. 


●Homoni ndio kishawishi cha nguvu za kiume mwilini. 


●Kukosa amino asidi huweza kusababisha kukosa hamu ya mapenzi au kupungukiwa na nguvu za kiume.



VITUNGUU SAUMU

●Vitunguu saumu vina allicin, kiambato kinachosaidia mzunguko mzuri wa damu kwenye viungo

vya uzazi. 


●Kuwa na mzunguko mzuri wa damu kwenye uume ni sababu kubwa ya kuongeza stamina katika tendo la ndoa.



NDIZI

●Kuwa na stamina ni muhimu katika ufanyaji mapenzi. 


●Ndizi ni chanzo kikubwa cha vitamin B ambayo husaidia sana katika kuongeza stamina na nguvu mwilini hasa wakati wa kufanya kazi nzito. 


●Ndizi ina kimeng’enyo cha Bromelain ambacho huongeza nguvu za kiume, ashki ya mapenzi

(libido).



MIZIZI YA MACA

●Maca Root Ni mmea maarufu sana huko Brazil ambao umekua ukitumiwa na wanaume na wanawake wengi ili kuwapa nguvu ya muda mrefu,kuondoa stress,afya ya uzazi,kubalance hormone,na kuwapa

hamu ya tendo la ndoa,n.k

N.k....

●Binafsi ninashauri kutumia njia asilia katika kutatua matatizo yako yote ya kiafya. Mwili una njia

zake za kurekebisha kila kitu. 


▪︎Ukiona kuna tatizo inaashiria kuna upungufu ambao unatakiwa

kurekebishwa. 


▪︎Kutumia madawa makali hudhoosha mwili na hivyo kuupunguzia uwezo wa

kufanya kazi kama inavyotakiwa. 


▪︎Ni vizuri kama utamuona daktari kama ukiona hakuna

kinachowezekana kabla hujaanza kutumia madawa.



📌Mara nyingi njia asilia hutumia muda mrefu kuleta mabadiliko, lakini matokeo yake hudumu zaidi kuliko kutumia madawa makali ambayo hu-BOOST na hayatibu.


Dr Liwaya

0755162724

Comments

Popular posts from this blog

ZIJUE FAIDA,MADHARA YA KITUNGUU SWAUMU KATIKA MWILI WA BINADAMU

MAGONJWA YANAYOTIBIKA KUPITIA KITUNGUU SAUMU Huyeyusha mafuta mwilini (kolestro) Husafisha njia ya mkojo na kutibu U.T.I Hutibu amoeba, minyoo na Bakteria wengine Huzuia kuhara damu (Dysentery) Huondoa Gesi tumboni Hutibu msokoto wa tumbo Hutibu Typhoid Huondoa mabaka mabaka kwenye ngozi Hutibu mafua na malaria Hutibu kifua kikuu (ukitumia kitunguu swaumu kesho yake unaweza kutokwa na makohozi mengi tu ambayo ni ishara kwamba kweli kinatibu kifua kikuu (TB) Hutibu kipindupindu Hutibu upele Huvunjavunja mawe katika figo Hutibu mba kichwani Huupa nguvu ubongo. Kazi nzuri niliyopenda zaidi katika kitunguu swaumu. Huzuia meno kung’ooka na kutuliza maumivu Huongeza SANA nguvu za kiume pia hutibu uanithi (kushindwa kusimama kabisa uume) Hutibu maumivu ya kichwa Hutibu kizunguzungu Hutibu shinikizo la juu la damu Huzuia saratani/kansa Hutibu maumivu ya jongo/gout Huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula Huongeza hamu ya kula Huzuia damu kuganda Husaidia kutibu kisukari Husaidia kutibu ...

TATIZO LA KUFUNGA CHOO NA KUPATA CHOO KIGUMU

Tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu ni jambo tunalolikwepa kwenye mazungumzo yetu ya kila siku. Hata hivyo ni tatizo kubwa katika jamii na mbaya zaidi wengi hawajuwi madhara yake ni nini ya kuendelea kulivumilia tatizo hili. Kupata choo kigumu au kufunga choo ni ishara ya tatizo lingine baya zaidi mwilini. Kama kuna jambo unapaswa uliepuke kwa nguvu zote basi ni hili. Kwa afya bora kabisa hakikisha unapata choo kila siku mara 2 hata mara 3. Choo kilaini siyo kigumu na chenye maumivu. Wakati mwingine utakapopata tatizo hili naomba usiwe na aibu kulisema wazi hata kwa boss wako ili upate matibabu kwa haraka. Kufunga choo au kupata choo kigumu ndiyo CHANZO KIKUU CHA UGONJWA WA BAWASIRI kwa waTanzania wengi na hii inachangiwa kwa sehemu kubwa kwa kula ugali wa sembe na kutokunywa maji mengi kila siku. Pamoja na hayo, hakuna ugonjwa rahisi kutibika kama huu ikiwa utaamua kushughulisha kichwa chako kidogo hasa kwa kuangalia unakula na kunywa nini kila siku. Inatakiwa ifahamike kuwa ...

UGONJWA WA KIHARUSI, CHANZO, DALILI NA TIBA YAKE ASILIA.

Pengine umekuwa ukisikia sehemu mbalimbali kuhusu tatizo la kiharusi lakini bado hukuwahi kusoma na kuelewa vizuri. Karibu katika mfululizo wa makala zetu ambapo utajifunza nini maana ya kiharusi, aina za kiharusi, nini chanzo ama visababishi vyake. jinsi gani upunguze hatari ya kupata ugonjwa huu na huduma ya dawa za virutubisho ambavyo vitakusaidia kuondoa athari za tatizo. Maelezo Ya Utangulizi Kwa Tatizo La Stroke Kiharusi au stroke hutokea bila kutoa kiashiria chochote. Na ndio maana kuchukua tahadhari za kuepuka kutokea kwa tatizo ni muhimu zaidi. Kwasababu endapo utapata kiharusi na kwa bahati njema mwili ukaendela kufanya kazi basi matokeo na madhara yake yatakusumbua sana maisha yote. Kuepuka madhara makubwa ya kiharusi mgonjwa anahitajika kutibiwa ndani ya saa moja baada ya kupata shambulizi. Hakikisha pia unafika haraka hospitali kama ukigundua moja ya dalili zifuatazo zimekutokea bila kutaraji. Kushindwa ghafla kutembea na kupoteza balansi ya mwili. Kuchanganyikiwa ghafla n...