Skip to main content

ZIFAHAMU SABABU ZINAZOWAFANYA MZUNGUKO WA HEDHI KUBADILIKA

Kwa kawaida, mizunguko ya hedhi hukaa kwa siku nne hadi saba. Kwa mfano matatizo ya mzunguko wa hedhi ni Pamoja na mizunguko ambayo hutokea chini ya siku 21 au Zaidi ya siku 35, ukakosa hedhi siku tatu au Zaidi, na mtiririko wa damu ya hedhi ambayo ni nyingi na ya muda mrefu sana au kutokwa na damu ya hedhi nyepesi kuliko kawaida.


Je, Mzunguko Wa Hedhi Wa Kawaida Ukoje?

Wanawake wengi wanapata kipindi cha hedhi ambacho huchukua siku nne hadi saba. Kipindi cha hedhi cha mwanamke kwa kawaida hutokea kila siku 28, lakini mzunguko wa kawaida wa hedhi unaweza kuanzia siku 21 hadi 35.

Mfano wa matatizo ya mzunguko wa hedhi ni kama hii:

  1. Vipindi vya hedhi ambavyo hutokea chini ya siku 21 au Zaidi ya siku 35
  2. Kukosa hedhi vipindi vitatu au mfululizo
  3. Kutokwa na damu nyingi ya hedhi au nyepesi kuliko kawaida
  4. Kipindi cha hedhi ambacho hukaa kwa muda Zaidi ya siku saba
  5. Vipindi vya hedhi ambavyo huambatana na maumivu, kichefuchefu au kutapika
  6. Kutokwa na damu ya hedhi mara mbili kwa mwezi au matone yad amu kujirudia mara kwa mara, au baada ya kukoma hedhi au baada ya tendo la ndoa

Mfano wa mzunguko wa hedhi usio wa kawaida ni Pamoja na:

  • Kukosa hedhi kabisa
  • Kupata damu ya hedhi na maumivu makali
  • Kutokwa na damu ya hedhi kwa muda mrefu
  • Kupatwa na damu ya hedhi mfululizo
Je, Nini Visababishi Vyake?

Kuna visababishi vingi vya vipindi vya hedhi visivyo vya kawaida, kuanzia msongo wa mawazo mpaka magonjwa mengine mbalimbali kama vile:
  1. Msongo wa mawazo
  2. Vidonge vya uzazi wa mpango
  3. Vivimbe kwenye mfuko wa uzazi(fibroid)
  4. Maambukizi katika via vya uzazi(PID)
  5. Vivimbe kwenye vifuko vya mayai
  6. Mayai kutokupevuka

Visababishi vingine vya mzunguko wa hedhi usio wa kawaida ni Pamoja na

  • Saratani ya kizazi au shingo ya kizazi
  • Matatizo ya tezi ya thyroid na kupelekea homoni kubadirika
  • Madhara yakiambatana na ujauzito au mimba kuharibika au kutunga nje ya kizazi
Je, Hali Ya Kubadirika Kwa Hedhi Hupimwaje?

Kama hali yoyote mzunguko wa hedhi imebadirika, unapaswa kuweka kumbukumbu ujue ni lini kipindi chako cha hedhi kilianza na kuisha, Pamoja na kiwango cha mtiririko na kama unatokwa na damu yenye mabonge. Weka alama ya dalili zozote zingine, kama vile kupata hedhi mara mbili kwa mwezi na hedhi yenye maumivu makali.

Kwahiyo daktari anaweza pia kuagiza upate vipimo hasa vifuatavyo:

  1. Vipimo vya damu ili kuona upungufu wad amu
  2. Uchafu unaotoka ukeni ili kuangalia maambukizi
  3. Kipimo cha ultrasound ili kuona kama kuna vivimbe vya fibroid au kwenye vifuko vya mayai(ovarian cysts)
  4. Kipimo ili kuona kama kuna tishu zimeota nje ya mfuko wa uzazi
Mpendwa msomaji naomba niishie hapa katika makala hii, na nikaribishe kipindi cha maswali na maoni yako.

Pia unaweza ukatuma namba yako ya WHATsAP tutakuunganisha na darasa letu uweze kupata masomo kila siku ya afya.

Je, Unahitaji Huduma? Basi unaweza kuwasiliana nasi kwa namba hizi: 0755162724 

Dar es salaam-Ilala Boma,

Karibu sana!

Comments

Popular posts from this blog

DAWA YA KUTIBU JINO UKIWA NYUMBANI

DAWA YA KUTIBU MENO KWA HARAKA NA UHAKIKA Dawa hii imeniponesha mm mwenyewe nilikuwa nasumbuliwa na jino la juu na ndipo nilipoamua kuandaa dawa hii na imenitibu kwa HARAKA na ufanisi wa Hall ya juu sana na bado sijapatapo kuona dawa nzuri kama hii,huna haja ya kung'oa meno yako baada ya kuifahamu dawa hii eti kwasababu yanauma Mahitaji 1.✍ Mafuta ya karafuu/clove oil. 2.✍ mafuta ya Nazi/coconut oil. 3.✍ Kitunguu maji. 4.✍ Kitunguu swaum. 5.✍ Pilipili manga. 6.Chumvi ya mawe/unga wake MAANDALIZI Ponda ponda Kitunguu maji,Kitunguu swaumu,chumvi ya mawe na pilipili manga kisha changanya na mafuta na Nazi na mafuta ya karafuu kwa kiasi kidogo (robo kijiko kidogo cha chai) kisha chukua mchanganyiko huu kisha uweke juani kwa muda wa dakika 15 kisha toa juani MATUMIZI 1.ikiwa jino lina tundu chukua uji uji wa mchanganyiko huu kisha weka katika tundu na mafuta yake yapakaae pembezoni mwa jino linalouma. 2.ikiwa jina halina tundu pakaa mafuta ya mchanganyiko huu pembezoni kulizunguka jino...

TATIZO LA KUFUNGA CHOO NA KUPATA CHOO KIGUMU

Tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu ni jambo tunalolikwepa kwenye mazungumzo yetu ya kila siku. Hata hivyo ni tatizo kubwa katika jamii na mbaya zaidi wengi hawajuwi madhara yake ni nini ya kuendelea kulivumilia tatizo hili. Kupata choo kigumu au kufunga choo ni ishara ya tatizo lingine baya zaidi mwilini. Kama kuna jambo unapaswa uliepuke kwa nguvu zote basi ni hili. Kwa afya bora kabisa hakikisha unapata choo kila siku mara 2 hata mara 3. Choo kilaini siyo kigumu na chenye maumivu. Wakati mwingine utakapopata tatizo hili naomba usiwe na aibu kulisema wazi hata kwa boss wako ili upate matibabu kwa haraka. Kufunga choo au kupata choo kigumu ndiyo CHANZO KIKUU CHA UGONJWA WA BAWASIRI kwa waTanzania wengi na hii inachangiwa kwa sehemu kubwa kwa kula ugali wa sembe na kutokunywa maji mengi kila siku. Pamoja na hayo, hakuna ugonjwa rahisi kutibika kama huu ikiwa utaamua kushughulisha kichwa chako kidogo hasa kwa kuangalia unakula na kunywa nini kila siku. Inatakiwa ifahamike kuwa ...

NI KWA NAMNA GANI BACTERIA (H.pyori) Husababisha vidonda vya TUMBO

-Bacteria, Helicobacter pylori/Campilobacter pylori_* anaweza kusafiri kutoka kwa mtu Mmoja kwenda kwa mwingine kupitia njia zifuatazo: ⤵⤵⤵ (a).📎Kupitia mate (kunyonyana midomo) (b).📎Kupitia matapishi. (c).📎 Kupitia kinyesi (d).📎Kupitia chakula ama maji yaliyokuwa na bacteria hawa. SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA MTU KUAMBUKIZWA BACTERIA HAWA_ (H.pylori) ⚫ Kuishi mazingira yenye mikusanyiko mkubwa wa watu bila kuchukua tahadhar. ⚫ Kunywa maji yasiyokuwa safi. ⚫ Kula vyakula visivyooshwa mfano matunda na Mboga za majani. ⚫ Kuishi karibu na mtu mwenye vidonda vya tumbo bila kuchukua tahadhar. H.pylori anapoingia katika mwili wa binadamu huathiri uzio mwenye kulinda ukuta wa tumbo na utumbo mdogo (protective mucous) hali hii hupelekea kudhoofika kwa kuta katika tumbo na utumbo mdogo. Ukuta huu unapodhoofika husababisha Tindikali (Asidi) inayozalishwa tumbo kuunguza na kuuchimba ukuta wa tumbo pia Bacteria hawa huchimba ukuta wa tumbo na KUSABABISHA kutokea vidonda katika ukuta wa tumbo...