Skip to main content

ZIFAHAMU SABABU ZINAZOWAFANYA MZUNGUKO WA HEDHI KUBADILIKA

Kwa kawaida, mizunguko ya hedhi hukaa kwa siku nne hadi saba. Kwa mfano matatizo ya mzunguko wa hedhi ni Pamoja na mizunguko ambayo hutokea chini ya siku 21 au Zaidi ya siku 35, ukakosa hedhi siku tatu au Zaidi, na mtiririko wa damu ya hedhi ambayo ni nyingi na ya muda mrefu sana au kutokwa na damu ya hedhi nyepesi kuliko kawaida.


Je, Mzunguko Wa Hedhi Wa Kawaida Ukoje?

Wanawake wengi wanapata kipindi cha hedhi ambacho huchukua siku nne hadi saba. Kipindi cha hedhi cha mwanamke kwa kawaida hutokea kila siku 28, lakini mzunguko wa kawaida wa hedhi unaweza kuanzia siku 21 hadi 35.

Mfano wa matatizo ya mzunguko wa hedhi ni kama hii:

  1. Vipindi vya hedhi ambavyo hutokea chini ya siku 21 au Zaidi ya siku 35
  2. Kukosa hedhi vipindi vitatu au mfululizo
  3. Kutokwa na damu nyingi ya hedhi au nyepesi kuliko kawaida
  4. Kipindi cha hedhi ambacho hukaa kwa muda Zaidi ya siku saba
  5. Vipindi vya hedhi ambavyo huambatana na maumivu, kichefuchefu au kutapika
  6. Kutokwa na damu ya hedhi mara mbili kwa mwezi au matone yad amu kujirudia mara kwa mara, au baada ya kukoma hedhi au baada ya tendo la ndoa

Mfano wa mzunguko wa hedhi usio wa kawaida ni Pamoja na:

  • Kukosa hedhi kabisa
  • Kupata damu ya hedhi na maumivu makali
  • Kutokwa na damu ya hedhi kwa muda mrefu
  • Kupatwa na damu ya hedhi mfululizo
Je, Nini Visababishi Vyake?

Kuna visababishi vingi vya vipindi vya hedhi visivyo vya kawaida, kuanzia msongo wa mawazo mpaka magonjwa mengine mbalimbali kama vile:
  1. Msongo wa mawazo
  2. Vidonge vya uzazi wa mpango
  3. Vivimbe kwenye mfuko wa uzazi(fibroid)
  4. Maambukizi katika via vya uzazi(PID)
  5. Vivimbe kwenye vifuko vya mayai
  6. Mayai kutokupevuka

Visababishi vingine vya mzunguko wa hedhi usio wa kawaida ni Pamoja na

  • Saratani ya kizazi au shingo ya kizazi
  • Matatizo ya tezi ya thyroid na kupelekea homoni kubadirika
  • Madhara yakiambatana na ujauzito au mimba kuharibika au kutunga nje ya kizazi
Je, Hali Ya Kubadirika Kwa Hedhi Hupimwaje?

Kama hali yoyote mzunguko wa hedhi imebadirika, unapaswa kuweka kumbukumbu ujue ni lini kipindi chako cha hedhi kilianza na kuisha, Pamoja na kiwango cha mtiririko na kama unatokwa na damu yenye mabonge. Weka alama ya dalili zozote zingine, kama vile kupata hedhi mara mbili kwa mwezi na hedhi yenye maumivu makali.

Kwahiyo daktari anaweza pia kuagiza upate vipimo hasa vifuatavyo:

  1. Vipimo vya damu ili kuona upungufu wad amu
  2. Uchafu unaotoka ukeni ili kuangalia maambukizi
  3. Kipimo cha ultrasound ili kuona kama kuna vivimbe vya fibroid au kwenye vifuko vya mayai(ovarian cysts)
  4. Kipimo ili kuona kama kuna tishu zimeota nje ya mfuko wa uzazi
Mpendwa msomaji naomba niishie hapa katika makala hii, na nikaribishe kipindi cha maswali na maoni yako.

Pia unaweza ukatuma namba yako ya WHATsAP tutakuunganisha na darasa letu uweze kupata masomo kila siku ya afya.

Je, Unahitaji Huduma? Basi unaweza kuwasiliana nasi kwa namba hizi: 0755162724 

Dar es salaam-Ilala Boma,

Karibu sana!

Comments

Popular posts from this blog

ZIJUE FAIDA,MADHARA YA KITUNGUU SWAUMU KATIKA MWILI WA BINADAMU

MAGONJWA YANAYOTIBIKA KUPITIA KITUNGUU SAUMU Huyeyusha mafuta mwilini (kolestro) Husafisha njia ya mkojo na kutibu U.T.I Hutibu amoeba, minyoo na Bakteria wengine Huzuia kuhara damu (Dysentery) Huondoa Gesi tumboni Hutibu msokoto wa tumbo Hutibu Typhoid Huondoa mabaka mabaka kwenye ngozi Hutibu mafua na malaria Hutibu kifua kikuu (ukitumia kitunguu swaumu kesho yake unaweza kutokwa na makohozi mengi tu ambayo ni ishara kwamba kweli kinatibu kifua kikuu (TB) Hutibu kipindupindu Hutibu upele Huvunjavunja mawe katika figo Hutibu mba kichwani Huupa nguvu ubongo. Kazi nzuri niliyopenda zaidi katika kitunguu swaumu. Huzuia meno kung’ooka na kutuliza maumivu Huongeza SANA nguvu za kiume pia hutibu uanithi (kushindwa kusimama kabisa uume) Hutibu maumivu ya kichwa Hutibu kizunguzungu Hutibu shinikizo la juu la damu Huzuia saratani/kansa Hutibu maumivu ya jongo/gout Huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula Huongeza hamu ya kula Huzuia damu kuganda Husaidia kutibu kisukari Husaidia kutibu ...

TATIZO LA KUFUNGA CHOO NA KUPATA CHOO KIGUMU

Tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu ni jambo tunalolikwepa kwenye mazungumzo yetu ya kila siku. Hata hivyo ni tatizo kubwa katika jamii na mbaya zaidi wengi hawajuwi madhara yake ni nini ya kuendelea kulivumilia tatizo hili. Kupata choo kigumu au kufunga choo ni ishara ya tatizo lingine baya zaidi mwilini. Kama kuna jambo unapaswa uliepuke kwa nguvu zote basi ni hili. Kwa afya bora kabisa hakikisha unapata choo kila siku mara 2 hata mara 3. Choo kilaini siyo kigumu na chenye maumivu. Wakati mwingine utakapopata tatizo hili naomba usiwe na aibu kulisema wazi hata kwa boss wako ili upate matibabu kwa haraka. Kufunga choo au kupata choo kigumu ndiyo CHANZO KIKUU CHA UGONJWA WA BAWASIRI kwa waTanzania wengi na hii inachangiwa kwa sehemu kubwa kwa kula ugali wa sembe na kutokunywa maji mengi kila siku. Pamoja na hayo, hakuna ugonjwa rahisi kutibika kama huu ikiwa utaamua kushughulisha kichwa chako kidogo hasa kwa kuangalia unakula na kunywa nini kila siku. Inatakiwa ifahamike kuwa ...

UGONJWA WA KIHARUSI, CHANZO, DALILI NA TIBA YAKE ASILIA.

Pengine umekuwa ukisikia sehemu mbalimbali kuhusu tatizo la kiharusi lakini bado hukuwahi kusoma na kuelewa vizuri. Karibu katika mfululizo wa makala zetu ambapo utajifunza nini maana ya kiharusi, aina za kiharusi, nini chanzo ama visababishi vyake. jinsi gani upunguze hatari ya kupata ugonjwa huu na huduma ya dawa za virutubisho ambavyo vitakusaidia kuondoa athari za tatizo. Maelezo Ya Utangulizi Kwa Tatizo La Stroke Kiharusi au stroke hutokea bila kutoa kiashiria chochote. Na ndio maana kuchukua tahadhari za kuepuka kutokea kwa tatizo ni muhimu zaidi. Kwasababu endapo utapata kiharusi na kwa bahati njema mwili ukaendela kufanya kazi basi matokeo na madhara yake yatakusumbua sana maisha yote. Kuepuka madhara makubwa ya kiharusi mgonjwa anahitajika kutibiwa ndani ya saa moja baada ya kupata shambulizi. Hakikisha pia unafika haraka hospitali kama ukigundua moja ya dalili zifuatazo zimekutokea bila kutaraji. Kushindwa ghafla kutembea na kupoteza balansi ya mwili. Kuchanganyikiwa ghafla n...