Skip to main content

ZIFAHAMU SABABU ZINAZOWAFANYA MZUNGUKO WA HEDHI KUBADILIKA

Kwa kawaida, mizunguko ya hedhi hukaa kwa siku nne hadi saba. Kwa mfano matatizo ya mzunguko wa hedhi ni Pamoja na mizunguko ambayo hutokea chini ya siku 21 au Zaidi ya siku 35, ukakosa hedhi siku tatu au Zaidi, na mtiririko wa damu ya hedhi ambayo ni nyingi na ya muda mrefu sana au kutokwa na damu ya hedhi nyepesi kuliko kawaida.


Je, Mzunguko Wa Hedhi Wa Kawaida Ukoje?

Wanawake wengi wanapata kipindi cha hedhi ambacho huchukua siku nne hadi saba. Kipindi cha hedhi cha mwanamke kwa kawaida hutokea kila siku 28, lakini mzunguko wa kawaida wa hedhi unaweza kuanzia siku 21 hadi 35.

Mfano wa matatizo ya mzunguko wa hedhi ni kama hii:

  1. Vipindi vya hedhi ambavyo hutokea chini ya siku 21 au Zaidi ya siku 35
  2. Kukosa hedhi vipindi vitatu au mfululizo
  3. Kutokwa na damu nyingi ya hedhi au nyepesi kuliko kawaida
  4. Kipindi cha hedhi ambacho hukaa kwa muda Zaidi ya siku saba
  5. Vipindi vya hedhi ambavyo huambatana na maumivu, kichefuchefu au kutapika
  6. Kutokwa na damu ya hedhi mara mbili kwa mwezi au matone yad amu kujirudia mara kwa mara, au baada ya kukoma hedhi au baada ya tendo la ndoa

Mfano wa mzunguko wa hedhi usio wa kawaida ni Pamoja na:

  • Kukosa hedhi kabisa
  • Kupata damu ya hedhi na maumivu makali
  • Kutokwa na damu ya hedhi kwa muda mrefu
  • Kupatwa na damu ya hedhi mfululizo
Je, Nini Visababishi Vyake?

Kuna visababishi vingi vya vipindi vya hedhi visivyo vya kawaida, kuanzia msongo wa mawazo mpaka magonjwa mengine mbalimbali kama vile:
  1. Msongo wa mawazo
  2. Vidonge vya uzazi wa mpango
  3. Vivimbe kwenye mfuko wa uzazi(fibroid)
  4. Maambukizi katika via vya uzazi(PID)
  5. Vivimbe kwenye vifuko vya mayai
  6. Mayai kutokupevuka

Visababishi vingine vya mzunguko wa hedhi usio wa kawaida ni Pamoja na

  • Saratani ya kizazi au shingo ya kizazi
  • Matatizo ya tezi ya thyroid na kupelekea homoni kubadirika
  • Madhara yakiambatana na ujauzito au mimba kuharibika au kutunga nje ya kizazi
Je, Hali Ya Kubadirika Kwa Hedhi Hupimwaje?

Kama hali yoyote mzunguko wa hedhi imebadirika, unapaswa kuweka kumbukumbu ujue ni lini kipindi chako cha hedhi kilianza na kuisha, Pamoja na kiwango cha mtiririko na kama unatokwa na damu yenye mabonge. Weka alama ya dalili zozote zingine, kama vile kupata hedhi mara mbili kwa mwezi na hedhi yenye maumivu makali.

Kwahiyo daktari anaweza pia kuagiza upate vipimo hasa vifuatavyo:

  1. Vipimo vya damu ili kuona upungufu wad amu
  2. Uchafu unaotoka ukeni ili kuangalia maambukizi
  3. Kipimo cha ultrasound ili kuona kama kuna vivimbe vya fibroid au kwenye vifuko vya mayai(ovarian cysts)
  4. Kipimo ili kuona kama kuna tishu zimeota nje ya mfuko wa uzazi
Mpendwa msomaji naomba niishie hapa katika makala hii, na nikaribishe kipindi cha maswali na maoni yako.

Pia unaweza ukatuma namba yako ya WHATsAP tutakuunganisha na darasa letu uweze kupata masomo kila siku ya afya.

Je, Unahitaji Huduma? Basi unaweza kuwasiliana nasi kwa namba hizi: 0755162724 

Dar es salaam-Ilala Boma,

Karibu sana!

Comments

Popular posts from this blog

UGONJWA WA NGIRI AU HERNIA

UGONJWA WA NGIRI AU HERNIA Hernia mara nyingi huwapata wanaume, Wengi waliokumbwa na ugonjwa huu hukosa tiba sahihi na kujikuta wanaangukia kwenye kufanyiwa upasuaji (Operation). Ugonjwa wa ngiri hujitokeza wakati sehemu ya utumbo inapoteleza na kupenya katika kiwambo cha msuli wa utumbo, na kuingia katika kende moja wapo, au sehemu ya juu ya paja. Pia hujitokneza pale kiwambo cha msuli unaotenganisha mapafu na utumbo kinapotoboka na kusababisha majimaji kwenye sehemu ya juu ya utumbo au sehemu ya chini ya mapafu. AINA ZA NGIRI Kutokana na tabia ya ugonjwa wa mshipa wa ngiri kujitokeza katika maeneo mbalimbali ya mwili, kwahiyo aina ya ngiri/Hernia hutegemea na sehemu ngiri ilipojitokeza: ▪️ Ngiri maji. -Hii ni aina ya ngiri ijulikanayo pia kwa kitaalamu kama (hydrocele) ▪️Ngiri kavu (Hernia). -Hujulikana pia kama ‘fermoral hernia’ kwa wanawake na huitwa ‘scrotal hernia’ kwa wanaume ▪️ Ngiri ya kwenye kifua - Hujulikana pia kitaalamu kama ‘hiatus hernia’ ▪️ Ngiri ya tumbo -hujulikana p...

MADHARA YA ZA KUBOOST NGUVU ZA KIUME

JE, KUNA MADHARA YOYOTE KUTUMIA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU KWA MUDA ? (DAWA ZA KOBOOST NGUVU KWA MUDA) Nimekuwa nikipokea swali hili ,"mimi natumia sana dawa kuboost au kunipa nguvu ninapohitaji kwenda kufanya mapenzi. Je, kuna madhara yoyote?." Mwingine anauliza .."samahan mimi nimetumia sana dawa za kunipa hamu wakati wa tendo la ndoa lakini saizi najikuta siwezi kabisa uume hauna nguvu hata nikitumia dawa nilizozoea kutumia bado sipati nguvu, je tatizo nini?" Mwingine huyu hapa, "Kila nikihitaji kufanya sex lazima nitumie mkongo ,au vumbi la kongo. Je wewe una dawa ya kutibu tatizo moja kwa moja mpaka nikawa na nguvu za kiume vizuri niachane na mkongo kabisa?" Jamani hayo hapo ni baadhi tu ya maswali mengi ninayoulizwa, na nimetambua kuwa zaidi ya wanaume 25,000 ambao nawapa elimu hii, idadi kubwa sana wamekumbwa na tatizo hili la uraibu (addiction) wa kutumia dawa za kuboost uwezo wa kufanya sex, wengine wanatumia vidonge vya kizungu kama Viagra, wengine ...

ZIFAHAMU FAIDA MUHIMU ZA ASALI

Asali inafahamika kwa muda mrefu kama chakula muhimu ambacho pia kinasaidia sana katika kupambana na magonjwa mbalimbali na matatizo yatokanayo na uzee. Kwa mujibu wa tafiti mpya za wataalamu wa madawa lishe na vifaa tiba, jarida la World News limeandika kuwa asali inauwezo mkubwa wa kutibu kama itachanganywa na mdalasini. Asali ikishachanganywa na mdalasini pamoja na mafuta ya vuguvugu ya mzaituni, hutoa kichocheo maridhawa cha kuotesha nywele kinachotumika katika dawa ya Dork ambapo mchanganyiko huo unapakwa kwa kusugua kichwani na kuachwa kwa dakika 15. Kwa mujibu wa watafiti wa madawa tiba, Dk Alexander Andreyed na Eric Vogelmann, amesema madhara yaletwayo na vyakula vyenye mafuta mwilini yanaweza kudhibitiwa kwa kiasi kikubwa kwa matumizi ya mara kwa mara ya chai iliyoungwa kwa kutumia mchanganyiko wa asali na mdalasini. Ugunduzi wao huo, uliyakinishwa vema kwenye jarida mashuhuri linalozungumzia masuala ya tiba la nchini Denmark la Julai 1994. Uchunguzi mwingine pia umeonesha kwa...